Sunday, February 23, 2014
Do you like this story?
FACEBOOK YASEMA ITAINUNUA WHATSAPP

Facebook na WhatsApp ni maarufu sana miongoni mwa
vijana.
Kampuni ya mtandao wa Kijamii ya Facebook imesema kuwa itanunua
mtandao wa mawasiliano ya ujumbe mfupi wa WhatsApp kwa kima cha dola bilioni
kumi na sita, na nyongeza zaidi ya dola bilioni tatu zitakazolipwa waanzilishi
wa mtandao huo pamoja na wafanyakazi wake.
Hiyo ndiyo biashara kubwa zaidi ya ununuzi kuwahi kutekelezwa na Facebook hadi kufikia sasa.
WhatsApp ni maarufu sana miongoni mwa vijana wanaotafuta kuepuka kulipia huduma ya kutuma ujumbe mfupi wa simu yaani SMS.
WhatsAp imeweza kuwasajili zaidi ya watumiaji milioni mia nne hamsini.
Katika taarifa, mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg amesema kuwa mtandao huo upo njiani kuwaunganisha watu bilioni moja jambo litafanya Facebook kuwa na thamani kubwa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ ”
Post a Comment