Saturday, March 8, 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI NA CHANGAMOTO TERE KWA AKINA MAMA WAJANE MBEYA.


Bi Sharfa akiwa na  baadhi ya watoto wake ambao ni mapacha nje ya nyumba yake ambapo watoto wake wengine wanaishi kwa shemeji yake.


Hii ni nyumba ya mama mjane ambayo aliachiwa ma mumewe ambaye alifariki kwa ajari ya pikipiki.


Mwenyeki wa serikali ya Mtaa wa Inyala Bw.Nelson Mahena akitoa maelekezo kwa mama mjane huyo mara baada ya kufika ofisini kwakwe.

Mama mjane akiwa na watoto wake mapacha ambapo alionyesha kububujikwa  na machozi kutokana na majonzi ya kufiwa na muwewe pamoja na mzigo alio nao



Licha wanawake Duniani Kote wakiwa katika kusherekea siku yao ambayo imeadhimishwa Machi 8 mwaka huu bado idadi kubwa ya wanawake mkoani mbeya wameendelea kuishi katika mazingira magumu mara  baada ya waume zao kufariki dunia kutokana na sababu mbalimbali na kuwa acha wakiwa wajane.

Katika tukio la kusikitisha Mkazi wa Inyala Kata ya Iyunga jijini Mbeya Bi.Sharifa Adam( 31) ambaye ni mama mjane mwenye watoto watano amejikuta katika hali ngumu ya kimaisha kufuatia mume wake kufariki dunia Februali 27 mwaka huu .

Akizungumza kwa masikitiko makubwa mama huyo amedai kuwa amekuwa akiishi katika mazingira magumu mara baada ya mume wake kufariki dunia na kumuachia mzigo mkubwa wa watoto watano huku yeye akiwa hana shughuli yoyote inayo muingiizia kipato.

Amesema mume wake alikuwa akijishughulisha na kazi ya Bodaboda katika kituo cha Iyunga ambapo katika  hali ya kusikitisha mumewe huyo aliuwawa na kundi la watu mara baada ya kumkodisha.

Amesema mara baada ya kupokea taarifa za kuuwawa kwa mumewe alichukua jukumu la kutoa taarifa katika kituo cha polisi Iyunga na kwa ndugu wa marehemu  ambapo ulianza msako kwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na bodaboda wenzake ambapo walifanikiwa kuukuta mwili wa mume wake  ukiwa umetelekezwa katika kijiji kimoja wilayani Mbozi.

Kwa mujibu wa maelezo ya mama huyo amedai kuwa mara baada ya jeshi la polisi kufanikiwa kuupata mwiii huo baadae pia pikipiki ya mume wake na watuhumiwa wote walitiwa mbaroni ambao kwa sasa kesi hiyo ipo kituo cha polisi kwa ajili ya upelelezi.

Mama huyo amesema wakati mume wake anafariki alimuachia watoto watano ambao kati yao watatu walikuwa wakisoma shule ya msingi Ikuti darasa la kwanza na la pili huku wawili wakiwa wachanga ambao ni mapacha hivyo maisha yake kwa sasa ni magumu sana na anahitaji msaada wa haraka vinginevyo atawapoteza watoto wake kutokana na tatizo la njaa.

 
Hata hivyo amedai kuwa  marehemu mume wake alimuachia nyumba yenye vyumba viwili ambayo bado hijakamilika  hivyo kumfanya aendelee kuishi ndani ya nyumba hiyo huku ikiwa haina madirisha na watato wake watano.

Kufuatia hali amewaomba wasamalia wema kujitokeza na kumsaidia mama huyo ambapo pia watoto wake waweze kwenda shule pamoja na mapacha hao kupata lishe bora.

Hata hivyo amelitaka Dawati la jinsia la wanawake na watoto mkoani humo kuhakikisha wanamsaidia kwa haraka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo hatimaye mahakamani na kutolewa kwa hukumu ili aweze kupata haki yake.

0 Responses to “MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI NA CHANGAMOTO TERE KWA AKINA MAMA WAJANE MBEYA.”

Post a Comment

More to Read