Wednesday, April 9, 2014
RC KANDORO:SHEREHE ZA MAONYESHO NANE NANE ZIMEKOSA UHALISIA.
Do you like this story?
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maonyesho ya nanenane ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw Abbas Kandoro akifungua kikao |
Wajumbe mbalimbali kutoka kanda za nyanda za juu kusini wakiwa wanamsikiliza kwa makini mwenyekiti |
Baadhi ya majengo yaliopo kwenye kiwanja cha John Mwakangale nanenane jijini Mbeya. |
Maandalizi ya uwanja wa nanenane wa John Mwakangale Jijini Mbeya. |
WAJUMBE wa
kamati ya sherehe za maonyesho ya wakulima(Nane Nane)Nyanda za Juu Kusini kwa
pamoja wamekubaliana kusimamisha tafrija za usiku wakati wa maonyesho hayo ili
kuimarisha ushiriki na kuboresha maonyesho hayo.
Tamko hilo
limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia
ni Mwenyekiti wa kamati hiyo kwenye kikao chwa maandalizi ya maonesho na
sherehe za wakulima Nane nane 2014 katika uwanja wa John Mwakangale Jijini
Mbeya.
Amesema,
kumekuwepo na utaratibu wa kufanyika kwa tafrija za siku za Mikoa
mara kiongozi anapomaliza kutembelea na kisha kufanya tathimini ya
shughuli nzima jambo ambalo limetajwa kuchangia washiriki kutoelewa
maana halisi ya sherehe hizo.
“Sioni umuhimu
wa kufanyika kwa tafrija husika kwani washiriki wamekuwa wakinywa pombe na kula
nyama ovyo na kuondoa maana halisi ya sherehe za wakulima,”amesema Kandoro.
Aidha, wakiunga
mkono tamko hilo baadhi ya wajumbe, wamesema kuwa uchunguzi umeonesha
kwamba maandalizi na ushiriki wa tafrija za usiku yanaathiri utekelezaji wa
shughuli za msingi pamoja na kutumia fedha na rasilimali watu.
Hata hivyo
mwenyekiti huyo, amesema viongozi wa kiserikali wataendelea na utaratibu wao wa
kukagua na kutembelea mabanda ya maonyesho kama kawaida kilichosimamishwa ni
tafrija za usiku.
Maonyesho ya
Nane Nane Nyanda za Juu kusini inayowakilisha mikoa ya Rukwa, Katavi, Njombe,
Iringa, Ruvuma na Mbeya yanatarajia kufanyika Agosti Mosi mwaka huu na mgeni
rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RC KANDORO:SHEREHE ZA MAONYESHO NANE NANE ZIMEKOSA UHALISIA.”
Post a Comment