Thursday, April 10, 2014
VIROBA VYA KONYAGI FEKI WAPANDISHWA MAHAKAMANI MOSHI.
Do you like this story?
MAHAKAMA ya hakimu
mkazi Moshi, leo imefurika mamia ya wananchi waliokwenda kushuhudia watuhumiwa
sugu wa utengenezaji wa konyagi feki na bidhaa nyingine mbalimbali na
kuzibandika nembo za TRA ambayo inadiwa kudhuru maelfu ya watanzania.
Hata hivyo mahakama ya
mkazi moshi imetoa kwa dhamana watuhumiwa hao nane ambao wanakabiliwa na tuhuma
za kutumia alama za biashara za makampuni mengine kwa nia ya kutapeli.na
kujipatia pesa kinyume cha utaratibu.
Watuhumiwa hao ni
Yusuph George, Richard Leonard, Preygod Urassa, Mohamed Rashid, Greyson
Jonathan, George Kisivani, Hagai Nelson na Jackson Shayo, ambao wanatuhumiwa
kwa pamoja kwa
kutumia kwa nia ya
kutapeli alama ya biashara ya Konyagi kinyume cha sheria huku wakijua wazi ya
kuwa alama hiyo ni ya kibiashara ya halali ya kampuni ya Tanzania Distilleries
Limited.
Watuhumiwa hawa wana
kesi mbalimbali ikiwemo ile ya kutumia nyaraka za mamlaka ya mapato nchini TRA
ikiwemo mihuri yenye namba za kodi ya mapato jambo ambalo linadaiwa kuikosesha
serikali mapato mengi.
Wakili wa serikali
Julius Semali ameiambia mahakama ya mkazi Moshi kuwa watuhumiwa hao ni hatari
na kwamba wanakabiliwa na kesi za namna hiyo maeneo mbalimbali hapa nchini.
Singida wana kesi ya
namna hii na ambayo itaendelea tena Aprili 30, 2014, Ilala
wanatafutwa na polisi kwa kukutwa na nyaraka za TRA wakati Arusha wanatafutwa
kwa kukiuka dhamana na kutoroka mwaka 2012.
Pamoja na kupewa
dhamana kwenye kesi hiyo huko Moshi, bado hakimu aliamuru warudishwe rumande
kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Kesi hii imevutia
mamia ya wakazi ambapo miongoni mwao ambao ni wafanyabiashara za mabaa wametoa
wito kwa wananchi kuepuka kunywa konyagi vichochoroni kutokana na madhara
ambayo wameshapata watu wengi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “VIROBA VYA KONYAGI FEKI WAPANDISHWA MAHAKAMANI MOSHI.”
Post a Comment