Thursday, July 17, 2014

TPDC YATOA UFAFANUZI MKATABA WA STATOIL.



Shirika la maendeleo ya petrol (TPDC) limetoa ufafanuzi kuhusu  mkataba wa uzalishaji wa gesi  asilia baina ya serikali  na kampuni ya mafuta ya statoil  likieleza kuwa walioanzisha   suala la kuwepo kwa ulaghai  hawakuelewa vizuri mikataba  hiyo.

Mkurugenzi mtendaji wa TPDC yona killagane aliwaambia waandishi  wa habari jana kuwa mkataba wake na statoil unaibeba zaidi  serikali kwa kupata sehemu kubwa ya mapato bila kuweka kiasi chochote cha pesa tofauti na ilivyoelezwa.

Hivi karibuni mwandishi mmoja alibainisha uwepo wa ulaghai  katika mkataba  huo akidai serikali itapoteza kati y ash 670  bilioni n ash 1.68 trilioni iwapo mapitio hayatafanyika  katika mkataba  huo ili  kuwanufaisha  wananchi.

Lakini kilangane alifafanua  kuwa mkataba  wa awali baina ya statoil  na serikali  unaotumia mfumo wa mgawanyo wa mapato wa MPESA ulibainisha kuwa  iwapo mafuta  yangegundulika na siyo gest statoil ilipendekeza serikali  kupata asilimia 30 ya mapato ya rasilimali hiyo na 70 ibaki  kwa kampuni hiyo.

Baada ya gesi kugunduliwa statoil na kamati ya majadiliano  ya serikali  walikaa tena mwaka 2012 kupanga upya kiwango cha mgawanyo wa mapato na walikubaliana serikali ingepata  asilimia 61 ya mapato baada ya kutoa gharma za uzalishaji na kilichobaki  kubaki kwa statoil amesema killagane.

Amesema mapato  ya serikali katika mkataba wa gesi hayajalishi kampuni  hiyo ilipata hasara au faida na kwamba kiwango Fulani cha rasilimali chenye thamani ya gharama za uzalishaji huwekwa  kando na kile kinachozidi ndicho kinachofawanywa  kama mapato.

Kuhusu sababu za mkataba  wa kutumia gesi uliofanyika baada ya kugundulika  rasilimali hiyo kaimu mkurugenzi  mtendaji wa TPDC  james andilile amesema MPSA haukuwa mkataba wa mwisho ndiyo maana mkataba wa kupatikana gesi ulifanyika  kuruhusu  makubalino mapya  ya kugawana mapato na hufanyika kwa kampuni zote za utafutaji mafuta.

0 Responses to “TPDC YATOA UFAFANUZI MKATABA WA STATOIL.”

Post a Comment

More to Read