Tuesday, July 8, 2014
WAKUFUNZI 33 WAPATIWA MAFUNZO MKOANI IRINGA.
Do you like this story?
Na Friday
Simbaya,
Jumla ya wakufunzi 33 kutoka wilaya za
Mufindi na Iringa Vijini wapatiwa mafunzo ya ushiriki wa wananchi katika
usimamizi wa maliasili (misitu na wanyamapori) katika mafunzo ya siku tisa
yaliofanyika mjini Iringa katika Ukumbi VETA, kuanzia tarehe 25/06 hadi 03/07
mwaka huu.
Mafunzo hayo yalishirikisha asasi nne
ambapo kwa wilaya ya Mufindi ni ASHTECH na MUVIMA na kwa Iringa vijijini ni
MJUMIKK na MBOMIPA pamoja na washiriki wengine 17 kutoka kata ambao nao watashiriki
kutoa mafunzo ya mradi wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili,
kama vilevile
maafisa tarafa, madiwani na maafisa maendeleo ya jamii, na Watendaji wa kata.
maafisa tarafa, madiwani na maafisa maendeleo ya jamii, na Watendaji wa kata.
Meneja wa mradi huo, Dkt. Naima Besta
alisema mafunzo hayo yameganyika katika sehemu nne ambapo mafunzo ya awali
yawakufunzi yalitolewa kwa timu ya mradi kutoka LEAT; mafunzo ya pili ni kwa
wakufunzi 33 kutoka wilaya ya Mufundi na Iringa vijini, mafunzo ya watendaji
wanaohusika na maliasili katika ngazi ya wilaya ambayo yatafuatiwa na mafunzo
ya wanakamati mbalimbali za maliasili katika ngazi ya vijiji na sehemu ya
mwisho ni mafunzo kwa wananchi wote katika vijiji 14 vilivyoko Mufindi na
Iringa vijijini.
Alisema kuwa mafunzo kwa ngazi ya
wilaya yatawahusisha maafisa wanyamapori, maafisa ardhi, maafisa misitu pamoja
na kamati mbalimbali za mazingira.
"Huu ni mradi wa ushiriki wa
wananchi katika usimamizi wa maliasili
unakusudia kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuisimamia serikali kutimiza wajibu wake katika kusimamia maliasili kwa kuwapatia elimu, nyenzo na mbinu zifaazoza kuwajibisha asasi za serikali zenye dhamana ya
usimamizi wa maliasili.
unakusudia kuwawezesha wananchi kushiriki katika kuisimamia serikali kutimiza wajibu wake katika kusimamia maliasili kwa kuwapatia elimu, nyenzo na mbinu zifaazoza kuwajibisha asasi za serikali zenye dhamana ya
usimamizi wa maliasili.
Mafunzo hayo ya Ufuatiliaji wa
Uwajibikaji Jamii ambao yanawalenga wananchi kujua kuwa ni haki yao kupata
ufafanuzi, uthibitisho na uhalalisho (3Us) juu ya namna ambavyo rasilimali za
umma zinavyosimamiwa na jinsi ambavyo rasilimali hizi hasa zinazotokana na
maliasili zinaendelea na zitaendelea kuhakikisha upatikanaji na ulindwaji wa
haki za msingi za binadamu. Lengo kuu nikuongeza ushiriki wa wananchi katika
usimamizi wa maliasili," alisema meneja wa mradi.
Naye mshiriki kutoka Asasi ya Mbomipa
Idodi na Pawaga wilayani Iringa, mwalimu Ngoola Mwangosi alishukuru shirika la
LEAT kwa kuwapatia mafunzo hayo ambapo alisema kuwa yamekuja wakati mwafaka
ambapo maeneo Hifadhi ya Taifa ya Ruaha inakabiliwa na tatizo la ujangili wa
tembo kwa sababu yatasaidia kupunguza vitendo katika maeneo ya hifadhi.
"Mafunzo haya yametujengea uwezo
wa kufahamu mwelekeo sahihi wa uwajibikahi jamii katika usimamizi wa maliasili
(misitu na wanyamapori)," alisema mwalimu Mwangosi.
Alisema kuwa mafunzo ya ufuatilaji wa
uwajibikaji jamii yamewajengea uwezo wa kutambua sheria na sera mbalimbali
zinazosimamia misitu na wanyamapori.
Mshiriki mwingine Gertrude Mkongwa kutoka
shirika la MUVIMA wilayani Mufindi alisema mafunzo hayo yamemsaidia kutoka
hatua moja hadi nyingine kwa sababu hakuwa na uelewa wowote kuhusu sheria na
sera mazingira, misitu na wanayamapori na maliasili kwa ujumla.
Mkongwa alisema kuwa mafunzo hayo
yamemuogeza uelewa juu ya zana za uwajibikaji na usimamizi jamii kwa kufuatilia
kila hatua ya mchakato.
Mradi wa Ushiriki wa wananchi katika
usimamizi wa maliasili unatekelezwa na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira
kwa Vitendo (LEAT) kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Maendeleo ya Kimataifa
la Marekani (USAID) kutoka kwa Watu wa Marekani.
la Marekani (USAID) kutoka kwa Watu wa Marekani.
Hivyo basi, LEAT ni asasi isiyokuwa ya
kiserikali inayofanya shughuli za ulinzi na usimamizi wa mazingira na
rasilimali nyingine kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na: Kuleta na kukuza
utawala bora wa usimamizi na ulinzi endelevu wa mazingira na maliasili kwa
kufungua na kuendesha kesi mahakamani zenye kupigania usimamizi na ulinzi mzuri
wa mazingiran na rasimali zake kwa masilahi ya watu na jamii.
Kufanya ushawishi na utetezi wa
mazingira na rasilimali zake, kufanya tafiti-mkakati zenye lengo la kuchagiza
usimamizi na ulinzi wa mazingira na rasilimali zake, kuwajengea uwezo wananchi
na kufanyakazi nao kwa pamoja na kimtandao, Kuwajibisha taasisi za serikali
zenye dhamana ya usimamizi mazingira na rasilimali zake,
Kupigania utunzaji na usimamizi mzuri
wa mazingira na rasilimali zake pamoja na ardhi na kupigania kuheshimiwa na
kufuatwa kwa ukamilifu sheria zote zinazohusika na usimamizi na ulinzi wa
mazingira, maliasili.
LEAT kwa kushirikiana na USAID
inatekeleza mradi huu wa ushiriki wa wananchi katika usimamizi na ufuatiliaji
wa maliasili ili kuboresha uwajibikaji wa serikali, taasisi na idara zake zenye
dhamana ya usimamizi wa maliasili ili kuwezesha usimamizi mzuri wa mazingira na
maliasili, mgawanyo wa haki wa faida na manufaa yatokanayo na maliasli, utawala
bora na utoaji wa huduma nzuri kwa jamii katika ngazi za wilaya, kata na vijiji
katika wilaya ambapo mradi huu unatekelezwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAKUFUNZI 33 WAPATIWA MAFUNZO MKOANI IRINGA.”
Post a Comment