Saturday, October 17, 2015
WANANCHI WADAIWA VITAMBULISHO VYA KURA KWA LAZIMA MOROGORO
Do you like this story?
Ikiwa imebaki siku chache kuelekea uchaguzi mkuu katika hali
isiyo ya kawaida watu wanne wasiofahamika itikadi zao za kisiasa wame kamatwa
na wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo(Chadema) kwa madai ya kupita
katika kata za manispaa ya Morogoro na kudai shahada za wapiga kura kwa nguvu
na kuanza kuorodhesha majina ya wananchi na namba zao za simu.
Wakizungumza baada ya kuwafikisha watu hao katika kituo cha
polisi viongozi wa Chadema akiwemo mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Morogoro
Jemsi Mkude wamesema watu hao walikuwa wakiwalaghai wananchi kwa kuandikisha
vyama vyao vya siasa, namba zao za shahada za kupigia kura, namba zao za simu
pamoja na kero zinazowakabili kwenye eneo hilo ambapo wamelitaka jeshi la
polisi kutenda haki ilikuepusha uvunjifu wa amani.
Kwa upande wananchi mashuhududa walio kumbana na watu hao
katika harakati za kuwaandikisha wapiga kura majina wameeleza jinsi watu hao
walivyokuwa wakifanya zoezi hilo kwa kudai kwa lazimima shahada za kupigia kura
ambapo baadhi ya watu walikubali na wengine waifa kwa afisa mtendaji wakata na
wananchi waliamua kuungana na kuwatia hatiani na kisha kuwapeleka katika kituo
cha polisi cha mji wa Morogoro.
Akitolea ufafanuzi kuhusiana na suala hilo msimamizi wa
uchaguzi jimbo la Morogoro mjini Bi Theresia Mahongo amesema kuwa kufanya hivyo
ni kosa la jinai na kwamba adhabu yake ni faini kati ya shilingi laki moja hadi
laki mbili au kifungo cha miaka miwili ama vyote na kuwaonya wananchi kuacha
kufanya hivyo nikosa la jinai.
Chanzo:ITV Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WANANCHI WADAIWA VITAMBULISHO VYA KURA KWA LAZIMA MOROGORO”
Post a Comment