Wednesday, September 13, 2017
Serikali kununua mashine za DNA
Do you like this story?
Serikali
imedhamiria kununua mashine tatu za vipimo vya vinasaba (DNA) ili
zitumike katika maabara za Kanda na hivyo kusogeza huduma karibu na
wananchi.
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeo ya Jamii, Jinsi, Wazee na
Watoto Dkt. Hamis Kigwangala wakati akijibu swali la Mbunge wa Chumbuni,
Ussy Pondeza kuhusu ucheleweshwaji wa matokeo ya uchunguzi wa sampuli
ikiwemo sampuli za makosa ya jinai.
Amesema
kuwa Serikali ina mkakati wa kuongeza mashine hizo ili kuwezesha
uchunguzi kufanyika kwa wakati kwa vielelezo vya makosa ya jinai ikiwa
ni pamoja na vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na watoto.
”
Sampuli za uhalali wa watoto kwa wazazi zinafanyika kwa wepesi zaidi
kuliko sampuli za makosa ya jinai kwani sampuli hizo zinachukuliwa moja
kwa moja toka kwa wahusika hivyo kurahisisha uchunguzi wake endapo
wahusika wa uchukuaji watachukua kwa umahiri na uhifadhi utafanyika kwa
namna stahili,” amesema Dkt. Kigwangala.
Aidha,
amesema kuwa sampuli za uchunguzi wa makosa ya jinai zinachukuliwa toka
maeneo ya matukio hivyo uchunguzi wake unaweza kuchukua muda zaidi
kutegemeana na aina ya sampuli na eneo zilipotoka.
Hata
hivyo, ameongeza kuwa Serikali inampango wa kuanzisha kituo cha kupima
vinasaba (DNA) Mkoani Mbeya kwa lengo la kupunguza ucheleweshaji wa
matokeo ya uchunguzi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Serikali kununua mashine za DNA”
Post a Comment