Thursday, April 10, 2014
AFISA MASOKO WA KAMPUNI YA COCA COLA AUAWA KWA KUMIMINIWA RISASI YA KIFUA MKOANI IRINGA.
Do you like this story?
NA FRANK
KIBIKI, IRINGA
WATU wawili
wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Iringa kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga
risasi, kifuani Afisa masoko wa kampuni ya Vinywaji ya Coca-Cola Mkoani Iringa,
Steven Mbwilo (40).
Kaim Kamanda wa
Jeshi hilo, mkoani Iringa Wakyo Nyigesa aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Pascal
Benedict (44), mkazi wa Tunduma na Selemani Juma (42) mkazi wa Soweto mkoani
Mbeya.
Alisema kuwa
tukio hilo limetokea juzi, saa sita mchana katika kijiji cha Mtiri, kata ya
Ifwagi, Wilayani Mufindi ambapo watu hao walimvamia afisa huyo na kumpiga
risasi iliyosababisha kifo chake papo hapo.
Hata hivyo,
walisema kuwa marehemu huyo baada ya kupekuliwa alikutwa na fedha Shilingi
Milioni 4.7 sambamba na simu yake ya mkononi.
Aliongeza kuwa
sababu za mauaji hayo hazijajulikana na kwamba, uchunguzi zaidi unaendelea ili
watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani kujibu shtaka linalowakabili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “AFISA MASOKO WA KAMPUNI YA COCA COLA AUAWA KWA KUMIMINIWA RISASI YA KIFUA MKOANI IRINGA.”
Post a Comment