Friday, April 11, 2014
ASKARI 10 WA USALAMA BARABARANI WAFUKUZWA KAZI.
Do you like this story?
JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama
Barabarani limewafukuza kazi askari wake 10 kwa kosa la kwenda kinyume cha
kanuni na sheria za jeshi hilo.
Akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama
Barabarani nchini, Mohamed Mpinga, alisema kuwa askari hao walipatikana
na hatia baada ya kufunguliwa mashitaka ya kijeshi.
Alisema: “Baada ya kufunguliwa mashtaka
yaliyokuwa yakiwakabili ya kwenda kinyume na mwenendo wa Jeshi la Polisi,
walipatikana na hatia hivyo wengine tuliwafukuza na wengine kuwabadilisha vituo
vyao vya kazi.”
Mpinga alisema wameamua kuwashughulikia
askari hao ili kurejesha imani kwa wananchi ambao baadhi yao wameanza kupoteza
imani wakiamini kuwa wapo askari wa barabarani wanaokiuka maadili ya jeshi
hilo, lakini wanalindwa.
Ingawa Kamanda Mpinga hakutaja makosa
ya askari hao, lakini habari za kipolisi kutoka ndani ya jeshi hilo wanadaiwa
kuwa walijihusisha na vitendo vya rushwa, kinyume cha maadili na sheria za
jeshi hilo.
“Hali hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa
utendaji wa kazi kuwa mgumu na jamii kutoamini kazi zinazofanywa na jeshi hilo,
ndiyo maana tumeamua kuchukua hatua kali na tutaendelea kufanya hivyo kwa
wengine wenye tabia hiyo,” alisema Mpinga.
Askari hao wamefukuzwa ikiwa ni siku
chache baada ya Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kutangaza
kuwafukuza kazi askari wake wanne kwa makosa ya utovu wa nidhamu, ikiwemo
kujihusisha na vitendo vya ujambazi.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, askari hao wanadaiwa
kushiriki kwenye tukio la ujambazi lililotokea Machi 9, mwaka huu, eneo la
Mbezi Beach baada ya kuvamia ofisi za Kampuni ya Kichina ya Hong Yang
inayojishughulisha na kazi za ujenzi.
>>>via tanzania daima
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ASKARI 10 WA USALAMA BARABARANI WAFUKUZWA KAZI.”
Post a Comment