Saturday, April 12, 2014
HALI YA HEWA YA TUKUYU YAWATATIZA VIJANA WA MABORESHO WA TAIFA STARS.
Do you like this story?
Meneja wa
Timu Ndugu Boniface Clemence akizunguzia juu ya maendeleo ya Kambi hiyo
|
Chuo cha Uwalimu Cha Msasani ambacho
uwanja wake unatumika kwa vijana hao
|
KIKOSI cha
Wachezaji 33 Cha timu ya maboresho ya Taifa Stars, kimeendelea vyema
katika kambi yake iliyoko Tukuyu
Wilayani Rungwe Mkoani mbeya katika Hotel ya Land Mark Hotel.
Uwanja unaotumika
na wachezaji hao kwa jaili ya mazoezi ni
katika Chuo Cha Ualimu Cha Msasani kilichopo hatua kadhaa toka katika
Hotel hiyo.
Akizungumza
na Blog hii Meneja wa Timu hiyo Ndugu Boniface Clemence amesema kuwa kambi ya
vijana hao inaendelea vyema licha ya kuwepo kwa changamoto za hapa na pale.
Amesema kwa
asilimia kubwa vijana hao wapo katika afya njema hasa kutokana na kupatiwa
huduma nzuri zilizopo kambini hapo.
Amesema
vijana hao wameonyesha nidhamu ya hali ya juu kwa kuonyesha ushirikiano kutoka
kwa viongozi wao.
Hata hivyo
Kocha Mkuu Ndugu Oscar Koloso amesema kuwa maendeleo ya vijana hao yako vizuri
licha ya kukumbana na hali ya hewa yenye baridi kali hali ambayo imewafanya
baadhi yao kuteteleka kidogo hasa kutokana na mazingira waliyotoka.
Amesema
changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni kutokana na mvua zinazoendelea
kunyesha kila siku hali ambayo inawafanya wafanye mazoezi na mvua hizo huku
siku nyingine kulazimika kufanya mazoezi ya kukimbia tu badala ya kuimgia
uwanjani.
Amesema kwa
sasa wapo katika hatua ya kufanya mazoezi magumu ya kukimbia na mpira kwani
mazoezi magumu ya viongo wamekwisha kamilisha.
Hata hivyo
Kocha huyo amebainisha kuwa wamejaribu kwenda haraka hasa kutokana na muda kuwa
mchache katika kambi hiyo ambayo kwa hatua ya kwanza wanatakiwa kukaa kwa
kipindi cha mwezi mmoja.
Wachezaji
waliobahatika kuingia kwenye mchakato huo wa maboresho ya Taifa Stars kuwa
ni Abdulaziz Khatib Haji (Mjini
Magharibi), Abubakar Abbas Ibrahim (Tanga), Benedicto Tinoko Mlekwa (Mara) na
Mtindi Kheri Ali (Kaskazini Unguja) ambao ni makipa.
Kwa upande wa
mabeki wa pembeni waliochaguliwa katika mchakato huo ambao upo chini ya
udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager ni Edward Peter Mayunga (Kaskazini
Pemba), Hussein Moshi (Tabora), Omari Kindamba (Temeke) na Shiraz Abdallah
(Ilala).
Mabeki wa
kati ni Abbas Ali Haji (Kaskazini Unguja), Ancy Abdon (Kagera), Emma Namwamba
(Temeke), Hussein Juma Akilimali (Njombe), Joram Nasson (Iringa), Kayombo
Silvanus Henrico (Ilala), Miraji Maka (Mwanza), Ramadhan Ame
Ramadhan (Kusini Unguja) na Said Juma Ali (Mjini Magharibi).
Viungo wapo
Abubakar Mohamed Ally (Kusini Unguja), Hashim Ramadhan Magoma (Shinyanga), Juma
Said Jega (Lindi), Mtenje Alban Juma (Tanga), Ryna Mgonyike (Temeke) na Yusuf
Mpilipili (Temeke).
Washambuliaji
ni Abdallah Kagumbwa (Temeke), Abrahman Othman Ally (Mjini Magharibi), Athanas
Fabian Bayagala (Mbeya), Athanas Mdamu (Mwanza), Ayubu Hashim Lipati (Ilala),
Chunga Said (Manyara), Mbwana Mshindo Mussa (Tanga), Michael David Mlekwa
(Lindi), Mohamed Seif Said (Kusini Pemba), Omar Athuman Nyenje (Mtwara), Paul
Michael Bundala (Ilala), Ramadhan Kapalamoto (Kinondoni) na Roman Nyapunda
(Temeke).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HALI YA HEWA YA TUKUYU YAWATATIZA VIJANA WA MABORESHO WA TAIFA STARS.”
Post a Comment