Saturday, April 19, 2014
IVO, CANNAVARO WATEMWA STARS, MAKIPA WOTE WA AZAM WACHUKULIWA.
Do you like this story?
Ivo Mapunda |
Cannavaro |
KOCHA Msaidizi wa Taifa Stars, Salum Mayanga amewaacha
kipa Ivo Mapunda wa Simba SC na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Yanga SC
katika kikosi chake cha wachezaji wengine 23 watakaoingia kambini kesho (Aprili
20 mwaka huu) kuungana na 16 waliotajwa awali kujiandaa kwa mechi ya kirafiki
dhidi ya Burundi itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu.
Mayanga amewaita makipa wote wa Azam FC, Aishi Manula na Mwadini Ally pamoja na Deogratias Munishi wa Yanga, wakati mabeki aliowachukua ni Abdi Banda (Coastal Union), Aidan Michael (Ruvu Shooting), Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Hassan Mwasapili (Mbeya City), Kelvin Yondani na Said Moradi (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Frank Domayo (Yanga),
Himid Mao (Azam) na Jonas Mkude (Simba).
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance), Haruna Chanongo (Simba), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Khamis Mcha (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Markhiya, Qatar), Ramadhan Singano (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance), Haruna Chanongo (Simba), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Khamis Mcha (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Markhiya, Qatar), Ramadhan Singano (Simba), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Wachezaji walioitwa kutoka katika kikosi cha maboresho ni kipa Benedicto Tinoko Mlekwa (Mara), mabeki wa kati; Emma Namwondo Simwanda (Temeke) na Joram Nason Mgeveje (Iringa). Walinzi wa pembeni ni Omari Ally Kindamba (Temeke), Edward Peter Mayunga (Kaskazini Pemba) na Shiraz Abdallah Sozigwa (Ilala).
Viungo ni Yusuf Suleiman Mlipili (Temeke), Said Juma Ally (Mjini Magharibi), Abubakar Ally Mohamed (Kusini Unguja), Hashim Ramadhan Magona (Shinyanga), Omari Athumani Nyenje (Mtwara) na Chunga Said Zito (Manyara).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “IVO, CANNAVARO WATEMWA STARS, MAKIPA WOTE WA AZAM WACHUKULIWA.”
Post a Comment