Monday, April 21, 2014
MBEYA CITY FC UTANI MWIKO, MAANDALIZI YA MSIMU UJAO YAIVA!!.
Do you like this story?
TAARIFA
zilizotufikia asubuhi ni kwamba benchi la ufundi la Mbeya City fc chini ya
kocha mkuu, Juma Mwambusi akisaidiwa na Maka Mwalwisyi linatarajia kufanya
kikao mchana wa leo kwa lengo la kutathmini walichovuna msimu huu.
Kocha
msaidizi wa Mbeya City, Maka Mwaliwisyi ameuambia mtandao huu kuwa
wamefurahishwa na mafanikio ya kushika nafasi ya tatu katika msimu wao wa
kwanza wa ligi kuu Tanzania bara, ingawa malengo yao ya kutwaa ubingwa
hayajatimia.
“Mchana wa
leo sisi kama benchi la ufundi tunakutana ili kutathmini kile tulichokipata”.
“ Kulikuwepo
na changamoto nyingi na tumemaliza nafasi ya tatu”.
“Tunakaa
kwasababu tunatakiwa kuwasilisha ripoti mapema ili kuendelea na maandalizi ya
timu”. Alisema Maka.
Kuhusu
usajili, Maka alisema hawatahangaika na wachezaji wenye majina kwasababu
falsafa yao inawabana.
“Wachezaji
wetu wanatutosha. Tutapata wengine kwa njia ile ile tuliyotumia”.
“ Falsafa
yetu inasema lazima tuwatoe wachezaji chini na kuwapandisha juu. Tukisema
tutamani basi tutapotea njia yeti tuliyoianzisha”
“Hawa
tulionao tutabaki nao ili tuone falsafa yetu itatufikisha wapi. Hatusajili
wachezaji wenye majina na ndivyo ilivyo kwa Mbeya City fc”. Aliongeza Maka.
Mbeya City
imekuwa timu bora msimu huu kwa kuleta changamoto kubwa kwa klabu za Simba,
Yanga na Azam fc.
Katika msimu
wake wa kwanza, wamewachomoa Simba katika nafasi tatu za juu.
Wamemaliza
ligi katika nafasi ya tatu kwa pointi 49, huku nafasi ya nne ikiangukia
mikononi mwa Simba kwa pointi 38.
Mwa jana,
Yanga walitwaa ubingwa, Azam fc nafasi ya pili, Simba nafasi ya tatu, Kagera
Sugar nafasi ya nne.
Lakini mwaka
huu Azam fc wametwaa ubingwa, nafasi ya pili Yanga, Mbeya City fc ya tatu,
Simba ya nne, na Kagera Sugar imeporomoka mpaka nafasi ya tano.
Timu nyingine
zilizopanda na Mbeya City fc, kwa maana ya Ashanti United na Rhino Rangers
zimeshashuka daraja sambamba na JKT Oljoro.
Sasa nafasi
zao zimechukuliwa na Stand United ya Shinyanga, Ndanda fc ya Mtwara na Polisi
Morogoro ya Mkoani Morogoro.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)



0 Responses to “MBEYA CITY FC UTANI MWIKO, MAANDALIZI YA MSIMU UJAO YAIVA!!.”
Post a Comment