Monday, April 21, 2014

MOYES MWENDO MDUNDO KUBOMOA REKODI ZA MAN UNITED!!.




MASHETANI wekundu, Manchester United wamekuwa na msimu mbaya mwaka huu tangu David Moyes aingie Old Traffod kurithi mikoba ya Sir Alex Ferguson na sasa anaendelea kuvunja rekodi mbalimbali klabuni hapo.

Baada ya kufungwa mechi ya jana mabao 2-0 na Everton uwanja wa Goodison Park, Man United hawawezi kumaliza ligi katika nafasi ya nne na kwa maana hiyo watakosa michuano ya UEFA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995.

Ushindi wa jana uliwafanya Everton kwa mara ya kwanza kushinda nje ndani dhidi ya Man United tangu mwaka 1969-70.
Hapo chini ni orodha ya rekodi zilizovunjwa na Moyes ambazo zilichapishwa na mtandao wa Goal.com baada ya Man United kulala mabao 3-0 dhidi ya Manchester City  mwishoni mwa mwezi machi mwaka huu, lakini Moyes amendelea kuvunja rekodi zingine msimu huu
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
United kwa mara kwanza wanamaliza ligi wakiwa nafasi ya chini tangu ligi kuu England kuanzishwa.
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
United wanashindwa kufuzu michuano ya UEFA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
United wamefanya vibaya zaidi nyumbani baada ya miongo kadhaa kupita
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Wamefungwa mara tatu mfululizo msimu huu tangu 2001.
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Wametolewa raundi ya tatu katika kombe ka  FA Cup  kitu kilichotokea mara moja wakati wa Ferguson
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Kufungwa kwa mara ya kwanza na Swansea City wakiwa Old Trafford.
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Kufungwa kwa mara ya kwanza nyumbani na Newcastle tangu mwaka  1972
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Kufungwa kwa mara ya kwanza nyumbani na West Brom tangu 1978
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Mechi ya kwanza ya ligi kupoteza dhidi ya Stoke tangu mwaka 1984
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Mara ya kwanza kwa Man United kufungwa bao la mapema zaidi ligi kuu –bao la Dzeko walipokabiliana na Manchester City
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Mara ya kwanza kwa Man City na Liverpool kumpiga nje ndani Man United Tangu Premier League kuanza
http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif

http://i1.goal.com/web/goal/2014.02.27-v1/images/default/match/g1big.gif
Mara ya kwanza Everton kumfunga Man United nje ndani tangu mwaka 969-70

0 Responses to “MOYES MWENDO MDUNDO KUBOMOA REKODI ZA MAN UNITED!!.”

Post a Comment

More to Read