Tuesday, April 22, 2014
MZEE AKATWA NYETI ILEJE.
Do you like this story?
Mkazi
wa Kijiji Mapogolo wilayani Ileje, London Haonga (61), amelazwa katika
Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya watu wanaodaiwa kuwa watatu kumkata sehemu za
siri usiku wa kuamkia juzi.
Haonga
alifikishwa hospitalini hapo juzi jioni baada ya kupata huduma ya kwanza kwenye
Hospitali ya Wilaya ya Ileje alikofikishwa akiwa taabani.
Akiwa
Hospitali ya Rufaa, jana hiyo mzee huyo hakuweza kusimulia lolote, lakini
wauguzi wa Wodi ya Kwanza alikolazwa walisema hali yake inaendelea vizuri
ingawa alikuwa na maumivu makali.
“Wamemkata
sehemu zote za siri zikiwamo korodani,’’ alisema muuguzi, ambaye hakutaka
kutajwa jina lake
Akizungumza
kwa simu, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mapogolo, Cosmas London alisema Haonga
alipatwa na mkasa huo saa 2.30 usiku wa kuamkia juzi baada ya watu wawili
kumvamia njiani na kumfunga kitambaa na hatimaye kumkata sehemu zake za siri.
Alisema
alipiga yowe kuomba msaada na majirani walifika na kutoa msaada wa kumpeleka
Hospitali ya Wilaya ya Ileje huku wakiwasaka watuhumiwa wa tukio hilo.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alisema jeshi lake linaendelea na
upelelezi na kuwasaka wahusika.
Msangi
alisema taarifa za awali zinawahusisha ndugu wa Haonga na kwamba upelelezi
unaendelea.
Kamanda
Msangi alitoa wito kwa jamii kuacha tabia za kujichukulia sheria mkononi na kwamba
wanapokuwa na migogoro ni vyema kutatua kwa njia ya mazungumzo ili kuleta
amani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MZEE AKATWA NYETI ILEJE.”
Post a Comment