Saturday, April 12, 2014
UFALME WA RAGE SIMBA WAFIKA KIKOMO, SWALI NANI KURITHI MIKOBA YAKE?, KAZI KWA WANACHAMA!!
Do you like this story?
KWA MUDA mrefu mashabiki na
wanachama wa Simba sc wamekuwa wakiamini kuwa klabu yao imefika hapo ilipo
kwasababu ya mwenyekiti wao Ismail Aden Rage kuongoza vibaya.
Rage amekuwa akisuguana na wanachama wake kwa muda mrefu, lakini sasa
ameshatangaza kutogombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi Mkuu unaotarajia
kufanyika mei 4 mwaka huu.
Rage alitangaza maamuzi hayo machi 16 mwaka huu katika mkutano mkuu wa
wanachama ulioitishwa maalumu kwa ajili
ya kufanya marekebisho wa katiba.
Kauli ya aina yake katika mkutano huo ilikuwa ile ya Rage kuwaita
wanachama wa Simba ni ‘mbumbumbu’
Kufuatia kauli hiyo, Rage, alilazimika kuwaomba radhi wanachama hao
zaidi ya 571 waliohudhuria mkutano huyo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la
Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
“Napenda kuwaomba radhi wanachama wenzangu kutokana na nilivyosema
tuache umbumbumbu, lakini sikuwa namaanisha kama wengi wenu mlivyoelewa,”
alisema Rage.
Licha ya kusema hatagombea tena uongozi, Rage, alisema ataendelea kuwa
mwanachama mwaminifu wa Simba na atatoa mchango wake ili kufanikisha maendeleo.
Ikumbukwe kuwa kabla ya kauli hiyo, Rage alishawahi kusema kauli za
aina yake.
Mwezi machi mwaka jana aliwahi kuuita
mkutano wa wanachama walioaminika kuwa zaidi ya 600 ambao ulitangaza
kumpindua madarakani kuwa ni kama `kikao
cha harusi`.
Pia novemba mwaka jana kamati ya utendaji ya Simba ilitangaza kumuondoa
madarakani mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage.
Kamati hiyo ilifikia uamuzi wa kumsimamisha Rage akiwa nje ya nchi na kumtangaza aliyekuwa Kaimu Makamu Mwenyekiti, Joseph Itang’are ‘Mzee Kinesi’ kushika nafasi hiyo ya juu zaidi katika klabu hiyo.
Mzee Kinesi alisema walifikia maamuzi hayo kutokana na mwenyekiti huyo kwenda kinyume na makubaliano na Kamati ya Utendaji ya Simba.
Lakini baadaye ya mwanaume huyo kurudi alitamba kuwa yeye ni mwenyekiti
halali wa Simba na kikao hicho kilikuwa kikao cha harusi.
Wakati anawasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere
kulikuwa na kundi kubwa la watu walioaminika kuwa wanachama wa Simba
waliojitokeza kumlaki na kumshangilia kwa nguvu.
Kweli jamaa alirudi na baadaye TFF walitangaza kumtambua kuwa ndiye
mwenyeki halali wa Simba, lakini wakamtaka aitishe mkutano wa dharura na
kumpangia ajenda.
Rage aligoma na kusema yeye ndiye mwenye mamlaka ya kupanga ajenda za
mkutano kwa mujibu wa katiba.
Yapo mengi ya kuyasema kuhusu Rage, lakini sasa ameshatangaza
kung`atuka baada ya muda mrefu wa mvutano na viongozi wenzake pamoja na
wanachama wa Simba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UFALME WA RAGE SIMBA WAFIKA KIKOMO, SWALI NANI KURITHI MIKOBA YAKE?, KAZI KWA WANACHAMA!!”
Post a Comment