Saturday, April 12, 2014
WATU 37 WAKAMATWA VURUGU ZA BODABODA MBEYA.
Do you like this story?
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi |
Watu
37 wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa mbeya kwa kosa la kufanya
fujo na kuharibu mali.
Akizungumzia
Tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi amesema kuwa tukio hilo
limetokea April 11 mwaka huu majira ya saa 10:30 asubuhi huko
katika eneo la iyela - airport, kata ya iyela, jijini
Mbeya ambapo kundi la watu wakiwemo waendesha pikipiki maarufu kwa
jina la bodaboda zaidi ya mia mbili walivamia kwenye msiba wa marehemu siza
john mwambenja [28] mwendesha pikipiki @ bodaboda, mkazi wa
airport na kufanya fujo ikiwa ni pamoja na kuharibu mali mbalimbali
katika nyumba hiyo.
Amesema
Lengo la Bodaboda hao ilikuwa kushinikiza kumkamata mtalaka wa marehemu Ndugu Oliva
herode mwamlima [ 25] mkazi wa forest mpya ambaye alikuwepo katika msiba
huo kwa madai kuwa anahusika na njama za mauaji ya aliyekuwa mume wake
kutokana na kuachwa kwa sababu za matatizo ya kifamilia.
Amesema
kuwa Marehemu Siza Johnjohn aliuawa na mtu/watu wasiofahamika na
mwili wake kukutwa umetupwa kando ya reli ya tazara tarehe 09.04.2014
ukiwa na jeraha la kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni na kando yake
kutelekezwa pikipiki yake mpya yenye namba za usajili t. 932 ctz
aina ya kinglion.
Kamanda
Msangi amebainisha kuwa Kufuatia vurugu hizo zilizozimwa na jeshi la polisi
mkoa wa mbeya, watu 37 walikamatwa na kufikishwa mahakama ya mwanzo mbeya mjini
ambao walisomewa mashitaka yao shauri la jinai namba 291/2014.
Watuhumiwa
wote wamepelekwa mahabusu gereza la ruanda ambapo kesi itaanza kusikilizwa 14.04.2014.
Aidha
katika vurugu hizo mali za jeshi la polisi gari moja la kituo cha polisi
kati 474 aina ya land rover 110 liliharibiwa kwa kupigwa mawe
na kuvunjwa kioo kikubwa cha mbele. Hakuna madhara ya kibinadamu yaliyoripotiwa
kutokea wakati wa vurugu hizo na hali ya amani ilirejea kuwa ya kawaida na
wananchi wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.
Kamanda
wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi ahmed z.
Msangi anatoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria
mkononi badala yake wahakikishe wanawafikisha katika mamlaka husika watuhumiwa
wanowakamata kwa tuhuma mbalimbali ili hatua za kisheria dhidi yao zichukuliwe.
Aidha
anatoa rai kwa jamii kujenga tabia ya kuheshimu mamlaka zilizowekwa
kisheria ikiwa ni pamoja na vyombo vya dola ili kuepuka matatizo yanayoweza
kuepukika badala ya kuleta ushindani na vurugu. Pia kamanda msangi amesisitiza
kuwa jeshi la polisi halitasita kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za
kisheria wale wote wanaokaidi na kuleta vurugu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATU 37 WAKAMATWA VURUGU ZA BODABODA MBEYA.”
Post a Comment