Thursday, May 15, 2014
PINDA ATANGAZA VITA NA MAMEYA,WENYEVITI WANAOKUZA MIGOGORO.
Do you like this story?
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda amesema ataanza kuwavua madaraka mameya na wenyeviti
watakaobainika kukuza migogoro ndani ya halmashauri zao kwa kuwa inachangia kwa
kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi.
Alitoa
rai hiyo jana wakati akifungua mkutano wa 30 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa
Tanzania (Alat) unaofanyika jijini hapa.
Amesema
baadhi ya mameya na wenyeviti wa halmashauri za wilaya wamekuwa wakiweka mbele
masilahi binafsi kwa kukuza migogoro na hatimaye muda mwingi kutumika kwenye
migogoro huku shughuli za maendeleo zikisimama.
“Mkigombana
wote tunawaondoa. Msiendekeze migogoro kwenye halmashauri zenu. Acheni kutumia
muda mwingi kulumbana na kugombana. Mnakuza mambo ambayo hayana masilahi kwa
maendeleo ya wananchi,” alisema Pinda.
Waziri
Mkuu alitoa mfano wa mgogoro uliosababisha meya wa Manispaa ya Bukoba
kujiuzulu, akisema kuwa ulimalizika baada ya mwenyewe kutangaza hivyo, lakini
baadaye madiwani wa kambi yake walienda mahakamani kuzuia vikao, jambo
lililosababisha fedha za maendeleo kushindwa kupelekwa.
Amesema
Tanzania ipo katika mkakati wa kuifanya iwe miongoni mwa nchi zenye uchumi bora
duniani ifikapo mwaka 2025 na sehemu kubwa ya maendeleo inatekelezwa katika
ngazi ya Serikali za Mitaa, hivyo ili kufikia lengo hilo hawezi kuvumilia kuona
baadhi ya mameya na wenyeviti wakikwamisha maendeleo kwenye maeneo yao.
Kuhusu
elimu, Pinda alisema kwenye shule za msingi kuna upungufu wa madawati 1,494,895
hivyo Alat inatakiwa kutokwepa jukumu hilo na kutumia fursa zilizopo
kuhakikisha yanachongwa.
“Hivi
Alat mnakubali aibu hii ya watoto wa wananchi wenu kukaa chini kwenye udongo?
Hii haikubaliki, lazima mtimize wajibu wenu wa kuhakikisha kila halmashauri
inayatengeneza,” alisema Pinda.
Pinda
pia aliiagiza Alat kutia msukumo kwenye ujenzi wa nyumba bora za wananchi ili
waondokane na kuishi kwenye nyumba zilizoezekwa nyasi.
Mwenyekiti
wa Alat, Dk. Didas Masaburi alisema wakati inatimiza miaka 30 jumuiya hiyo
imefanikiwa mambo mengi, ikiwamo kusimamia matumizi ya fedha za maendeleo
zinazotolewa na Serikali na wadau wa maendeleo kwenye halmashauri nchini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “PINDA ATANGAZA VITA NA MAMEYA,WENYEVITI WANAOKUZA MIGOGORO.”
Post a Comment