Wednesday, May 14, 2014
WAZAZI MKOANI NJOMBE WATAKIWA KUWAPA MAHITAJI WANAFUNZI NA SI KUENDEKEZA ULEVI TU
Do you like this story?
Imeelezwa kuwa wazazi na walezi wengi
mkoani Njombe wamekuwa wakithamini zaidi unywaji pombe kuliko kuwatimizia
mahitaji watoto wao wanaosoma elimu ya awali na msingi, jambo linalochangia
kudidimiza elimu kwa wanafunzi hao.
Hayo yamebainika katika kikao cha chama
cha waalimu wa awali Tanzania (TPTO) mkoa wa Njombe na waalimu wa shule za
awali na msingi kilichofanyika hii leo katika ukumbi wa kata ya Iwawa wilayani
Makete.
Akichangia katika kikao hicho Mwalimu
Frida Sanga kutoka shule ya msingi Makete amesema elimu ya Tanzania bado ina
mapungufu kwa kuwa wanadharau elimu ya awali ambayo ndiyo yenye msingi wa elimu
"Unakuta hata waalimu wanaofundisha madarasa ya awali hawathaminiwi,
wanaonekana kama hawafanyi kitu chochote kile, msingi wa elimu upo kwa watoto
hawa wa awali na hao waalimu wanaowafundisha wanatakiwa kuheshimiwa na kuungwa
mkono na jamii nzima na serikali kwa ujumla na si kuwapuuza" amesema.
Kwa upande wake mwl Vintan Mbilinyi
kutoka shule ya Msingi Maleutsi ameitaka serikali kuwa na ukaribu zaidi na
waalimu wa elimu ya awali huku akiwashauri waalimu wanaosoma hivi sasa kusomea
kufundisha madarasa ya chini badala ya kukimbilia madarasa ya juu
"Hawa vijana wa siku hizi hawataki
kufundisha madarasa ya chini mfano darasa la awali au la kwanza na badala yake
wanataka kuanzia la tano na kuendelea kwa kuwa hawataki shida, sisi
tunaofundisha madarasa haya ya chini tuna shida sana" amesema
Mwenyekiti wa chama chicho cha TPTO
mkoa wa Njombe Mwl. Magreth Nyika amesema ni kweli elimu ya awali ina
changamoto nyingi hivyo ni wajibu wao kwa pamoja kujiunga kwenye chama chao ili
nao watambulike na washirikiane kwa pamoja kutatua changamoto zinazowakabili.
Naye katibu wa chama hicho Mwalimu
George Mjema amesema upo umuhimu wa waalimu kufanya semina kwa wazazi kuwaeleza
ili waone tabu wanayowapa watoto wao pindi wanaposhindwa kuwahudumia na kuwapa
mahitaji yote ya shuleni huku wengi wa wazazi wao wakionekana kuendekeza
unywaji pombe.
Chama hicho cha TPTO mkoa wa Njombe
kinaendelea kuwakusanya wanachama katika wilaya zote za mkoa huo kikiwa na
kauli mbiu "sauti zetu zisikilizwe" ambapo mpaka sasa kina zaidi ya
wanachama 114
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WAZAZI MKOANI NJOMBE WATAKIWA KUWAPA MAHITAJI WANAFUNZI NA SI KUENDEKEZA ULEVI TU ”
Post a Comment