Friday, June 13, 2014
13 Jun 2014 BRAZIL YAIPA DOZI CROATIA MECHI YA UFUNGUZI KOMBE LA DUNIA, YAIPIGA 3-1
Do you like this story?
Neymar alifunga mabao mawili Brazil iipoilaza Croatia 3-1 |
Neymar akishangilia
bao lake la kwanza. WACHEZAJI Neymar na Oscar wamepeleka
vilio Croatia baada ya kuipa ushindi wa mabao matatu timu yao ya Brazil kwenye
mechi ya ufunguzi wa Fainali za Kombe la Dunia 2014 zinazofanyika nchini
Brazil.
Croatia walikuwa wa kwanza kupata bao
katika dakika ya 11 ambalo ni la kujifunga likiwekwa kimiani na beki Marcelo wa
Brazil.
Baadaye wenyeji Brazil walikuja juu na
kusawazisha bao hilo kupitia kwa mchezaji wao mahiri anayefananishwa na Pele,
Neymar kwa shuti la mbali lililomuacha mlinda mlango wa Croatia, Stipe
Pletikosa katika dakika ya 29 ya kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili Neymar aliipatia
Brazil bao la pili kwa mkwaju wa penalti ambao kipa Pletikosa alijaribu
kuupangua lakini ukajaa wavuni na kuwapa wenyeji ushindi wa 2-1 dakika ya 71.
Mchezaji wa Chelsea, Oscar alihitimisha
furaha ya waandaaji fainali hizo kwa bao lake la tatu dakika ya 90 ya mchezo.
Mpaka mwisho, Brazil 3, Croatia 1.
Leo michuano hiyo itaendelea ambapo Cameroon
watavaana na Mexico, Uholanzi wakikwaana na Hispania huku Chile
wakipepetana na Australia.
VIKOSI NA ALAMA ZAO
Brazil: Julio Cesar 6; Dani
Alves 5.5, Thiago Silva 6, Luiz 6, Marcelo 5.5, Paulinho 6 (Hernanes 63, 6),
Gustavo 7, Hulk 6 (Bernard 68, 6), Oscar 7, Neymar 8 (Ramires 88), Fred 6.5.
Benchi: Jefferson,
Fernandinho, Dante, Maxwell, Henrique, Willian, Jo, Maicon, Victor.
Mabao: Neymar 29,71
penalti, Oscar 90.
Kadi za njano: Neymar, Gustavo
Croatia: Pletikosa 6, Srna
6.5, Corluka 7, Lovren 6.5, Vrsaljko 6; Modric 7, Rakitic 7, Perisic 6.5,
Kovacic 6 (Brozovic 62, 5), Olic 6, Jelavic 6.
Benchi: Zelenika, Pranjic, Vukojevic,
Schildenfeld, Rebic, Sammir, Vida, Eduardo, Subasic.
Mabao: Marcelo 11
(kujifunga)
Kadi za njano: Corluka, Lovren.
Mchezaji Bora wa mechi: Neymar.
Refa: Yuichi Nishimura (Japan) 5.
Mashabiki: 61,000
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ 13 Jun 2014 BRAZIL YAIPA DOZI CROATIA MECHI YA UFUNGUZI KOMBE LA DUNIA, YAIPIGA 3-1 ”
Post a Comment