Sunday, June 8, 2014
MAHAKAMA YAONDOA KINGA YA WABUNGE.
Do you like this story?
Dar es
Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imefungua milango kwa mawaziri na
wabunge kufunguliwa mashtaka kutokana na kauli watakazozitoa bungeni ambazo ni
kinyume cha Katiba na Sheria.
Mahakama
Kuu ilitoa msimamo huo jana wakati ikitoa uamuzi wa pingamizi la awali katika
kesi ya kikatiba iliyokuwa ikimkabili Waziri Mkuu Mizengo Pinda,
lililowasilishwa na Jopo la Mawakili wa Serikali wakiongozwa na Naibu
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (DAG, George Masaju.
Kesi
hiyo namba 24 ya mwaka 2013 ilifunguliwa na Kituo cha Msaada wa Kisheria na
Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika
(TLS), dhidi ya Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), aliyeunganishwa
kama mlalamikiwa wa pili.
LHRC
na TLS walikuwa wakidai kuwa Pinda alivunja Katiba kutokana na kauli aliyoitoa
bungeni, wakidai kuwa ni amri kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria kuwapiga
wananchi wakati wa vurugu.
Hivyo,
walikuwa wakiiomba mahakama, pamoja na mambo mengine, itamke kuwa kauli hiyo ni
kinyume cha Katiba na imwamuru Pinda aifute hadharani.
Hata
hivyo, Pinda na AG waliokuwa wakitetewa na DAG Masaju akisaidiana na Mawakili
wa Serikali Wakuu (PSA, Gabriel Malata, Alecia Mbuya na Sarah Mwipopo),
waliweka pingamizi la awali dhidi ya kesi hiyo, wakitoa hoja tano za kuomba
kesi hiyo itupiliwe mbali.
Miongoni
mwa hoja hizo ni pamoja na kwamba kesi hiyo ni batili na iko mahakamani isivyo
halali kwa kuwa inakiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977 na Sheria
ya Mamlaka, Kinga na Haki za Wabunge, ya mwaka 1988.
Mawakili
hao walidai kuwa Pinda analindwa na Katiba Ibara ya 100 (1) na (2), ambazo
zinamkinga mbunge kushtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kwa
jambo lolote alilolisema, au alilolitenda, au alililoliwasilisha bungeni kwa
njia ya maombi, muswada au hoja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAHAKAMA YAONDOA KINGA YA WABUNGE.”
Post a Comment