Sunday, June 8, 2014

MAHAKAMA YAONDOA KINGA YA WABUNGE.



Dar es Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imefungua milango kwa mawaziri na wabunge kufunguliwa mashtaka kutokana na kauli watakazozitoa bungeni ambazo ni kinyume cha Katiba na Sheria.

Mahakama Kuu ilitoa msimamo huo jana wakati ikitoa uamuzi wa pingamizi la awali katika kesi ya kikatiba iliyokuwa ikimkabili Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lililowasilishwa na Jopo la Mawakili wa Serikali wakiongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali (DAG, George Masaju.

Kesi hiyo namba 24 ya mwaka 2013 ilifunguliwa na Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), dhidi ya Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), aliyeunganishwa kama mlalamikiwa wa pili.

LHRC na TLS walikuwa wakidai kuwa Pinda alivunja Katiba kutokana na kauli aliyoitoa bungeni, wakidai kuwa ni amri kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria kuwapiga wananchi wakati wa vurugu.

Hivyo, walikuwa wakiiomba mahakama, pamoja na mambo mengine, itamke kuwa kauli hiyo ni kinyume cha Katiba na imwamuru Pinda aifute hadharani.

Hata hivyo, Pinda na AG waliokuwa wakitetewa na DAG Masaju akisaidiana na Mawakili wa Serikali Wakuu (PSA, Gabriel Malata, Alecia Mbuya na Sarah Mwipopo), waliweka pingamizi la awali dhidi ya kesi hiyo, wakitoa hoja tano za kuomba kesi hiyo itupiliwe mbali.

Miongoni mwa hoja hizo ni pamoja na kwamba kesi hiyo ni batili na iko mahakamani isivyo halali kwa kuwa inakiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977 na Sheria ya Mamlaka, Kinga na Haki za Wabunge, ya mwaka 1988.

Mawakili hao walidai kuwa Pinda analindwa na Katiba Ibara ya 100 (1) na (2), ambazo zinamkinga mbunge kushtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kwa jambo lolote alilolisema, au alilolitenda, au alililoliwasilisha bungeni kwa njia ya maombi, muswada au hoja.

0 Responses to “MAHAKAMA YAONDOA KINGA YA WABUNGE.”

Post a Comment

More to Read