Monday, June 9, 2014
MVUTANO MKALI BUNGE,MAHAKAMA.
Do you like this story?
Kitendo
cha Mahakama kufungua milango kwa mawaziri na wabunge kufunguliwa mashtaka
kutokana na kauli watakazozitoa bungeni ambazo ni kinyume cha Katiba na Sheria,
kimeonekana kuwachanganya viongozi hao ambao wamesema kuwa wanalindwa na sheria
ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.
Wamesema
licha ya kuwa kazi ya Mahakama ni kutafsiri sheria, Bunge kutunga na Serikali
kusimamia sheria, nchi nyingi duniani wabunge wake wana kinga na hawashtakiwi
kwa kauli watakazozitoa bungeni.
Kauli
za wabunge hao zimekuja ikiwa imepita siku moja tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar
es Salaam, kutoa msimamo huo wakati ikitoa uamuzi wa pingamizi la awali katika
kesi ya kikatiba iliyokuwa ikimkabili Waziri Mkuu Mizengo Pinda,
lililowasilishwa na Jopo la Mawakili wa Serikali wakiongozwa na Naibu Mwanasheria
Mkuu wa Serikali (DAG, George Masaju.
Kesi
hiyo namba 24 ya mwaka 2013 ilifunguliwa na Kituo cha Msaada wa Kisheria na
Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika
(TLS), dhidi ya Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), aliyeunganishwa
kama mlalamikiwa wa pili.
Mahakama
Kuu katika uamuzi wake juzi ilikubaliana na baadhi ya hoja za mawakili wa
utetezi (Serikali) na kuitupilia mbali kesi hiyo, lakini ikatamka kuwa wabunge
na mawaziri wanaweza kushtakiwa kwa kauli au jambo walilolitamka bungeni,
linalokiuka sheria na haki za binadamu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MVUTANO MKALI BUNGE,MAHAKAMA.”
Post a Comment