Monday, June 9, 2014

MVUTANO MKALI BUNGE,MAHAKAMA.



Kitendo cha Mahakama kufungua milango kwa mawaziri na wabunge kufunguliwa mashtaka kutokana na kauli watakazozitoa bungeni ambazo ni kinyume cha Katiba na Sheria, kimeonekana kuwachanganya viongozi hao ambao wamesema kuwa wanalindwa na sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.

Wamesema licha ya kuwa kazi ya Mahakama ni kutafsiri sheria, Bunge kutunga na Serikali kusimamia sheria, nchi nyingi duniani wabunge wake wana kinga na hawashtakiwi kwa kauli watakazozitoa bungeni.

Kauli za wabunge hao zimekuja ikiwa imepita siku moja tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kutoa msimamo huo wakati ikitoa uamuzi wa pingamizi la awali katika kesi ya kikatiba iliyokuwa ikimkabili Waziri Mkuu Mizengo Pinda, lililowasilishwa na Jopo la Mawakili wa Serikali wakiongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali (DAG, George Masaju.

Kesi hiyo namba 24 ya mwaka 2013 ilifunguliwa na Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), dhidi ya Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), aliyeunganishwa kama mlalamikiwa wa pili.

Mahakama Kuu katika uamuzi wake juzi ilikubaliana na baadhi ya hoja za mawakili wa utetezi (Serikali) na kuitupilia mbali kesi hiyo, lakini ikatamka kuwa wabunge na mawaziri wanaweza kushtakiwa kwa kauli au jambo walilolitamka bungeni, linalokiuka sheria na haki za binadamu.

0 Responses to “MVUTANO MKALI BUNGE,MAHAKAMA.”

Post a Comment

More to Read