Mbunge wa Tunduru, Mtutura Mtutura (CCM).
Mbunge
wa Viti Maalum, Suzan Kiwanga (Chadema), amewaumbua wabunge wenzake kuwa
wanapeana na kuchukua rushwa ndani ya Bunge.
Suzan
aliyasema hayo juzi jioni wakati akichangia katika mkutano wa Chama cha Wabunge
walio katika Mapambano dhidi ya Rushwa (APNAC). Suzan alisema vitendo hivyo vya
rushwa vilionekana wakati wabunge hao walipokuwa wakiwachagua wabunge wa Bunge
la Afrika Mashariki.
“Rushwa
ilikuwa ni wazi wazi ukienda chooni unapewa laki mbili (Sh200,000)
unaondoka,”alisema Suzan.
Alisema
wao kama viongozi ambao wanatunga sheria na wanatakiwa kuisimamia serikali
wanapaswa kuwa waadilifu. Hata hivyo, Mbunge wa Njombe Kaskazini, Deo Sanga
(CCM), alisema hakuna ukweli kuhusu jambo hilo la baadhi ya wabunge kuchukua
rushwa hadi chooni.
Hata
hivyo, Mbunge wa Tunduru, Mtutura Mtutura (CCM), alimuunga mkono Suzan na
kusema suala hilo ni la kweli na kwamba kama Sanga hakuliona walikuwa
wanamkimbia.
|
0 Responses to “WABUNGE WAUMBUANA KUPOKEA RUSHWA BUNGENI.”
Post a Comment