Monday, June 9, 2014
0 09 Jun 2014 WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAM WAONEKANA WAKIOGA NA KUWAPIKIA WANAMGAMBO HAO
Do you like this story?
Mamia ya
wasichana waliotekwa na kundi la Boko Haram nchini Nigeria wanadaiwa kuonekana
wakioga na kuwapikia wanamgambo wa kundi hilo.
Aidha
taarifa zinaeleza wengi wa wasichana hao wanashikiliwa katika kambi tatu
tofauti nje ya Nigeria.
Mmoja wa
viongozi wanaohusika katika majadiliano ya kutaka wasichana hao waachiliwe
huru, Dk Steven Davis alikaririwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza
(BBC) akieleza hayo.
Dk Davis,
ambaye ni raia wa Australia na wenzake walio katika harakati za
kuwakomboa mabinti hao, waliwaona baadhi ya wasichana hao wakioga na upande
mwingine walikuwa wakiwapikia watekaji ambao ni kundi la wanamgambo wa
Boko Haram.
Davis
alisema majadiliano ya kutaka kuachiliwa kwa wasichana hao yalikuwa katika
hatua za mwisho kufanikiwa lakini makamanda wa kundi hilo walipinga wazo hilo
dakika za mwisho wakihofia kukamatwa.
Hata
hivyo, alisema juhudi zozote za kuwanusuru wasichana hao kwa nguvu hazitafua
dafu isipokuwa kwa njia ya mazungumzo na makubaliano ya amani.
Mei 14,
Serikali ya Nigeria ilieleza kuwa ipo tayari kufanya mazungumzo na kundi hilo
kuwezesha kuachiwa kwa wasichana hao zaidi ya 200.
Waziri wa
Elimu, Tanimu Turaki, alisema serikali ipo tayari kwa mazungumzo. Alisema kuwa
waliamua hatua hiyo itumike kwa kuwa utekaji huo umeibua hali ya hofu kuhusu ulinzi
wa wanafunzi katika shule mbalimbali nchini humo.
Baada ya
utekaji huo, Boko Haram walijinadi kuwa, watawauza mabinti hao kama watumwa.
Rais Goodluck Jonathan alipitisha kuwaachia wafungwa wao lakini waziri huyo
alisema imekuwa vigumu kujadiliana.
Hata
hivyo, Serikali ilisema njia zote za kuwapata wasichana hao ziko mezani
na wapo tayari kwa majadiliano lakini kundi hilo limekuwa likibadili uamuzi
mara kwa mara.
Boko Haram
ilionesha katika video inayosadikiwa kuwa ni ya wasichana hao, kundi la mabinti
takribani 130 wakiwa wamevaa vazi za kiislamu la hijabu lakini hawakueleza
video hiyo imechukuliwa wapi na lini.
Wasichana
hao wakiwa mchanganyiko, wakristo na waislamu walitekwa na kundi hilo usiku wa
Jumatatu, Aprili 14 mwaka huu katika hosteli ya shule mjini Chibok, Jimbo la
Borno.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ 0 09 Jun 2014 WASICHANA WALIOTEKWA NA BOKO HARAM WAONEKANA WAKIOGA NA KUWAPIKIA WANAMGAMBO HAO ”
Post a Comment