Wednesday, June 11, 2014
TAIFA STARS MZIGONI LEO KUWAWINDA `BLACK MAMBAS` KUSAKA TIKETI YA MOROCCO
Do you like this story?
IKIWA ni harakati
ya kuikabili Msumbiji `Black Mambas` katika mchezo wa mwisho kuwania kupangwa
hatua ya makundi kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika, AFCON
mwakani nchini Morocco, Taifa stars inatarajia kuingia tena kambini leo (Juni
11) mwaka huu.
Julai 20 mwaka
huu, Taifa Stars itaanza nyumbani uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na wiki
mbili baadaye itasafiri kwenda mjini Maputo kucheza mechi ya marudiano. Mshindi
wa jumla ataingia hatua ya mwisho ya makundi.
Stars
inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa na kambi ya siku tatu
jijini Dar es Salaam ikijumuisha wachezaji 28. Kwa mujibu wa programu ya Kocha
Mart Nooij, Stars itaingia tena kambini Juni 24 mwaka huu.
Wachezaji
wanaotakiwa kuripoti kambini ni Deogratias Munishi, Aishi Manula, Benedictor
Tinoko, Kelvin Yondani, Said Moradi, Nadir Haroub, Joram Nason, Shomari
Kapombe, Oscar Joshua, Edward Charles, Aggrey Morris na Pato Ngonyani.
Wengine ni
Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said
Juma, Haruna Chanongo, Himid Mao, Said Ndemla, John Bocco, Simon Msuva, Kelvin
Friday, Ramadhan Singano, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Mwegane Yeya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TAIFA STARS MZIGONI LEO KUWAWINDA `BLACK MAMBAS` KUSAKA TIKETI YA MOROCCO”
Post a Comment