Wednesday, June 11, 2014
YAYA TOURE AIMARIKA KWA KASI KUWAONESHA KAZI JAPAN MECHI NYA UFUNGUZI
Do you like this story?
Majeruhi: Yaya Toure, akiwa mazoezini jumatatu, anaendelea kuimarika kwa kasi kuelekea mchezo wa ufunguzi. |
KIUNGO
wa Ivory Coast,Yaya Toure anaendelea kuimarika kwa kasi kuelekea katika mchezo
wa ufunguzi wa kombe la dunia dhidi ya Japan jumamosi, amesema kocha Sabri
Lamouchi.
Toure
ameshindwa kufanya mazoezi ya pamoja na wenzake tangu alipofanyiwa upasuaji
mwezi uliopita.
Lamouchi
amesema timu ya madaktari wa Ivory Coast inajitahidi sana kuhakikisha
mchezaji huyo bora wa mwaka wa Afrika anacheza wakati nchi yake itakapoanza mchezo
wa ufungizi wa kundi C dhidi ya Japan mjini Recife.
'Tunafanya
kila linalowezekana ili acheze" kocha aliwaambia waandishi wa habari.
Toure
alipata majeruhi katikati ya mwezi aprili mwaka huu, lakini alirudi uwanjani
kuisaidia Manchester City kutwaa ubingwa wa pili katika misimu mitatu.
Halafu
akaenda Qatar kwa ajili ya matibabu na baadaye alijiunga na kikosi cha Ivory
Coast kwenye kambi ya mazoezi huko America.
Toure
hakucheza mechi mbili za kupasha pasha dhidi ya Bosnia na El Salvador.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “YAYA TOURE AIMARIKA KWA KASI KUWAONESHA KAZI JAPAN MECHI NYA UFUNGUZI”
Post a Comment