Friday, June 6, 2014
TFF: HATUJAFUTA MATUMIZI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI
Do you like this story?
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) limepokea taarifa za kutolewa
wito bungeni wa kulitaka litumie tiketi za elektroniki katika kukusanya
mapato.
wito bungeni wa kulitaka litumie tiketi za elektroniki katika kukusanya
mapato.
Tunataka ieleweke wazi kwa umma wa
Watanzania kuwa si nia yetu
kuchelewesha matumizi ya uingiaji mpirani kwa tiketi za elektroniki. Ieleweke
kuwa mfumo wa kuingia kwenye mbuga, KCMC, mipakani ni tofauti na uingiaji
mpirani.
kuchelewesha matumizi ya uingiaji mpirani kwa tiketi za elektroniki. Ieleweke
kuwa mfumo wa kuingia kwenye mbuga, KCMC, mipakani ni tofauti na uingiaji
mpirani.
Katika mpira wa miguu wanaingia maelfu
ya watu katika kipindi kifupi. Kwa kuzingatia umuhimu wa kulinda usalama wa
watazamaji na miundombinu ya viwanja ndio maana tulisitisha matumizi ya tiketi
za elektroniki hadi tujihakikishie usalama wa matumizi yake.
Tunafanya jitihada kwa karibu na
mzabuni benki ya CRDB ili kuhakikisha mfumo huu unaanza kutumika mara moja.
Kwa niaba ya sekta ya michezo tunatoa
wito kwa Serikali kushusha au kuondoa kodi kubwa zinazotozwa kwenye vifaa vya
michezo, hasa vinavyotumiwa na watoto kuanzia umri wa miaka 6-12, ili watoto
wetu waweze kuvipata kirahisi toka kwa wazazi wao ili waweze kujifunza kucheza
michezo kisasa tangu wakiwa wadogo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “TFF: HATUJAFUTA MATUMIZI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI”
Post a Comment