Tuesday, July 15, 2014
APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUJERUHI NA KUMTEMBEZA UCHI MWENZAKE MBELE ZA WATU
Do you like this story?
ZAITUNI Ally (30) mkazi wa manispaa ya
Morogoro amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa
Morogoro kwa tuhuma za kujeruhi na kumdhalilisha mwanamke mwenzie kwa
kumtembeza mtupu mbele za watu.
Akisoma maelezo ya shitaka hilo,
Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Aminata Mazengo alidai mbele ya Hakimu
Nuruprudensia Nassari kwamba mtuhumiwa huyo alitenda makosa mchana wa Julai 5
mwaka huu eneo la Msamvu B.
Ilidaiwa kwamba bila halali na akijua
kufanya hivyo ni kosa kisheria, mshtakiwa alimkata Rehema Juma na kitu chenye
ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia maumivu.
Mwendesha mashataka huyo aliendelea
kudai mahakamani hapo kwamba siku hiyo hiyo mtuhumiwa alimdhalilisha majeruhi
huyo kwa kumlazimisha kutembea mtupu mbele za watu.
Hata hivyo, mtuhumiwa alikana makosa
hayo na yupo nje kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapotajwa tena Julai 24 mwaka
huu kwa kuwa upelelezi haujakamilika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUJERUHI NA KUMTEMBEZA UCHI MWENZAKE MBELE ZA WATU ”
Post a Comment