Tuesday, July 15, 2014
PRISONS YAIONYA MBEYA CITY.
Do you like this story?
Tanzania prisons |
Mbeya City Fc |
Mbeya.
Timu ya Tanzania Prisons imeapa kuondoa uteja kutoka kwa Mbeya City msimu ujao
na kusisitiza kwamba vijana wa timu hiyo wanajinoa kisawasawa kuondokana na
hali hiyo.
Kocha
msaidizi wa timu hiyo, Shaban Kazumba, ambaye amejiunga na timu hiyo hivi
karibuni, alisema pamoja na msimu uliopita Mbeya City kuifunga Prisons mechi
zote mbili, msimu ujao mambo yatabadilika na kuitaka Mbeya City kutambua hilo.
Kazumba
alisema kwa sasa timu ina vijana wadogo ambao imewapandisha daraja kutoka timu
B, na kusajili wengine wawili waliokuwa huru kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi
Kuu na kwamba inafanya mazoezi katika Uwanja wa Sokoine kila siku.
“Tumeamua
kuwapandisha daraja kutoka U-20 kuja kuitumikia timu yetu kwa msimu ujao kwa
sababu tumeona wamekuwa na uwezo wa kupambana pindi wawapo uwanjani, lakini pia
tumesajili wachezaji wawili waliokuwa huru na sasa wataichezea timu yetu kwa
mkataba,” alisema Kazumba.
Wachezaji
waliopandishwa daraja ni pamoja na kipa Beno
Kakolanya,
Mfaume Omary, Frank William, Said Mtupa, Jacob Mwakalobo na Lambary
Sybianka.Alisema wachezaji waliokuwa huru na sasa wamesajiliwa na timu hiyo ni
pamoja na James Josephat na Meshack Olest, na kwamba Tanzania Prisons ina jumla
ya wachezaji 28 na sasa dirisha la usajili wa awali limefungwa.
Hiyo
ni moja ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ambayo sasa
imesogezwa mbele siku ya kuanza.
Awali
michuano hiyo ilikuwa ianze Agosti 24, lakini sasa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF) wameisogeza mbele na itaanza Septemba 20.
Sababu
za mbalimbali zilitajwa na TFF katika uamuzi huo, ambapo pia ni kupisha
michuano ya Kombe la Kagame.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “PRISONS YAIONYA MBEYA CITY.”
Post a Comment