Monday, July 14, 2014
SIMBA YASHUSHA WAWILI KWA MKUPUO.
Do you like this story?
SIMBA
inamaliza mazoezi ya gym leo Jumatatu na kuanzia jioni itageukia mazoezi ya
uwanjani kwa siku saba kabla ya kwenda Zanzibar kupiga kambi ukiwa ni mkao wa
Ligi Kuu na Maadhimisho ya Simba Day Agosti 8.
Lakini
jioni ya leo itashusha kwenye uwanja wa Chuo Kikuu wachezaji wawili wapya,
mshambuliaji Michael Mgimwa na Jabiri Aziz ‘Stima’ huku ikiendelea kumalizana
na wengine.
Mgimwa
ni mchezaji aliyelelewa na kituo cha TFF na baadaye alienda kucheza Thailand
wakati Stima ni mchezaji huru baada ya kutemwa na Azam FC. “Tuna nafasi mbili
za wachezaji wa kigeni na mbili wachezaji wazawa, hao watafanya mazoezi na
Simba ili kocha aone viwango vyao maana hatuwezi kusajili bila kujua mchezaji
ana kiwango gani na hatuwezi kusema moja kwa moja kama watachukuliwa ama
wataachwa mpaka kocha aridhike,” alisema Said Tuliy ambaye ni mjumbe wa Kamati
ya Usajili.
Simba
Ijumaa ilitangaza kumaliza usajili wake ndani ya saa 48 kwa maana ya hadi
kufikia jana Jumapili, lakini ikashindikana kutokana na wachezaji wao wengi
kudai dau kubwa ambalo haliendani na thamani zao. Vile vile kocha ametaka
kuwaona mazoezini kabla ya kuwasainisha.
Habari
kutoka ndani ya Kamati ya Mashindano zinasema kwamba baada ya mechi ya Simba
Day itakayochezwa jijini Dar es Salaam, kikosi kitakwenda kuweka kambi yake nje
ya nchi ambapo mpaka sasa bado wapo katika mchakato wa wapi wakaweke kambi hiyo
ingawa kuna mapendekezo ya kwenda Oman.
“Tunataka
Simba ifanye vizuri msimu ujao ndiyo maana yote haya yanatakiwa kufanywa mapema
ili tusiwe na maandalizi ya zima moto, ni kwa sababu tunataka kuwa na msimu
bora,” aliongeza kiongozi huyo.
“Tunasubiri
watu wa Kamati ya Usajili wamalize kazi yao ya kusajili ili tutakapokwenda
Zanzibar kikosi kiwe kimekamilika, ndiyo maana mazoezi yetu ya hapa yanachukuwa
kama siku saba na tutakwenda Zanzibar kwa kambi ya awali ya maandalizi ya Simba
Day.”
Kuhusu
wachezaji wao wa kigeni mabeki Joseph Owino na Donald Mosoti, alisema: “Owino
anaingia Jumatano (keshokutwa) lakini Mosoti bado haijafahamika kwani
mawasiliano ni magumu ingawa tunasikia yupo Uarabuni.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SIMBA YASHUSHA WAWILI KWA MKUPUO.”
Post a Comment