Monday, July 14, 2014
WAFANYAKAZI 20 WALIORUDI KINYEMELA TRL, WATAKIWA KUONDOKA HARAKA.
Do you like this story?
Zaidi
ya wafanyakazi 20 wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) ambao walipunguzwa kazi
mwaka 2007 na kulipwa stahiki zao kwa mujibu wa sheria, baadae wakarudi kwa
mgongo wa nyuma na kufanya kazi tena mpaka leo, wanatakiwa kuondoka mara moja
katika shirika hilo.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba katika mkutano na wafanyakazi wa shirika hilo, kujua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wafanyakazi hao.
Bwana Tizeba alisema kuwa wafanyakazi hao walirudi kwa mgongo wa nyuma na kuanza kufanya kazi wakati walishapunguzwa hawatakiwi kuendelea kufanya kazi katika shirika hilo, kwani wao ndio watakuwa chanzo kikubwa cha migogoro katika shirika hilo.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Charles Tizeba katika mkutano na wafanyakazi wa shirika hilo, kujua changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wafanyakazi hao.
Bwana Tizeba alisema kuwa wafanyakazi hao walirudi kwa mgongo wa nyuma na kuanza kufanya kazi wakati walishapunguzwa hawatakiwi kuendelea kufanya kazi katika shirika hilo, kwani wao ndio watakuwa chanzo kikubwa cha migogoro katika shirika hilo.
Aidha
alisema kuwa mishahara itapanda na reli itakarabatiwa kuanzia Tabora hadi Dar
es Salaam ili kurahisisha usafiri kwa abiria mbalimbali wanaotumia usafiri huo.
Shirika hilo kwa sasa linakabiliwa na uchakavu wa miundombinu ya reli, viti vya kwenye mabehewa vimechoka, mabehewa machakavu pamoja na vichwa vyake.
Shirika hilo kwa sasa linakabiliwa na uchakavu wa miundombinu ya reli, viti vya kwenye mabehewa vimechoka, mabehewa machakavu pamoja na vichwa vyake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAFANYAKAZI 20 WALIORUDI KINYEMELA TRL, WATAKIWA KUONDOKA HARAKA.”
Post a Comment