Friday, August 15, 2014

RAIS JACOB ZUMA AMTEUA BINTI YAKE MWENYE MIAKA 25 KUSHIKA WADHIFA WA JUU SERIKALINI .


Thuthukile Zuma


Thuthukile Zuma amehamishwa kutoka katika nafasi ya afisa uhusiano wa umma (Public Liaison officer) na kupandishwa cheo ndani ya miezi miwili akiwekwa katika nafasi muhimu na yenye nguvu " Mkuu wa wafanyakazi"  katika wizara ya huduma za posta na mawasiliano

Raisi wa africa ya kusini Jacob Zuma ameshutumiwa kwa kuwa  na mfumo wa upendeleo (Nepotism) baada ya kumteua mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 25 kushikilia cheo kikubwa serikalini.

Thuthukile ni mtoto wa mwisho katika watoto wanne wa Zuma, ambae alipokea degree ya heshima ya Anthropology na kukabidhiwa cheo hicho mwezi wa tano mwaka huu baadaya baba yake (Raisi Zuma)  baada yakuchagua baraza lake la mawaziri.

0 Responses to “ RAIS JACOB ZUMA AMTEUA BINTI YAKE MWENYE MIAKA 25 KUSHIKA WADHIFA WA JUU SERIKALINI .”

Post a Comment

More to Read