Saturday, August 16, 2014
WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA KWA KUPIGWA RISASI ENEO LA SIRARI MPAKANI MWA TANZANIA NA KENYA.
Do you like this story?
Watu zaidi ya nane kutoka nchi jirani ya Kenya wakishirikiana
na watanzania ambao wanadhaniwa kuwa ni majambazi wakiwa na silaha za kivita
wamevamia baa moja katika mpaka wa Tanzania na Kenya Sirari na kuwaua watu
wawili kwa kuwapiga risasi huku wakijeruhi wateja wengine watatu pamoja
na kupora kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa wateja hao na kukusanya
mauzo yote ya baa hiyo ya New mzalendo.
Baadhi ya wananchi ambao wameshuhudia tukio hilo wamesema
kuwa watu hao wamevamia baa hiyo wakiwa wamevalia nguo ambazo mara nyingi
zimekuwa zikitumiwa na askari wa jeshi la polisi na kuanza kurusha ovyo risasi
kisha kupora wateja walikuwa katika baa hiyo kabla ya kuingia kaunta na kupora
kiasi kikubwa chafedha.
Kamanda wa polisi wa kanda maalum ya Tarime na Rorya
kamishina msaidizi Lazaro Mambosasa, akizungumza na ITV kwa njia ya simu,
amekiri kutokea kwa tukio hilo, huku akisema majambazi hayo zaidi ya
manene toka nchi jirani wakishirikiana na watanzania wamefanya
uhalifu huo kwa kutumia bunduki za kivita aina ya smg huku akiwataja watu
walioawa kuwa Samwel Bhoke na mwingine ambaye amejulikana kwa jina moja
la Leonard wote wakazi wa Sirari.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA KWA KUPIGWA RISASI ENEO LA SIRARI MPAKANI MWA TANZANIA NA KENYA.”
Post a Comment