Tuesday, September 16, 2014
BABA AWAFUNGIA WATOTO NDANI MIEZI 10, WASHINDIA MLO MMOJA, MTOTO MMOJA AFA.
Do you like this story?
Mwanaume mmoja mkazi
wa Kijiji cha Msimba wilayani Uvinza, Kigoma, anashikiliwa na Polisi akidaiwa
kufungia watoto wake wanne ndani ya nyumba na kuwashindisha njaa kwa takribani
miezi 10.
Ofisi ya Ustawi wa
Jamii, Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, iliwabaini watoto hao hivi karibuni
kijijini Sunuka, wilayani Uvinza. Kati yao, watatu ni wa kiume.
Mkubwa ana umri wa
miaka minane akifuatiwa na msichana mwenye umri wa miaka saba. Wengine wana
umri wa miaka sita na minne.
Hayo yalithibitishwa
na Ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Penina Mbwete
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kumtaja baba
mzazi wa watoto hao kuwa ni Mateso Hassan (35).
Tayari baba huyo
anashikiliwa na Polisi ambapo awali ilikuwa katika Kituo cha Ilagala kabla ya
kuhamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi mjini Kigoma wakati akisubiri kupandishwa
kizimbani kusomewa tuhuma za kudaiwa kuwafungia watoto hao na kuwazuia kwenda
shule huku wakipata mlo mmoja tu, tena usiku wa manane.
Mjomba wa watoto hao,
Sunday Zuberi (38) alidai mama mzazi wa watoto, Yauzia Zuberi (38) alipigwa na
mumewe na kuamua kukimbia akiwa na mtoto mwingine mdogo mwenye umri wa mwaka
mmoja, ambaye pia alifariki baada kuugua na kukosa matibabu sahihi.
Alisema kwa
kushirikiana na ndugu wengine na baadhi ya wanakijiji cha Msimba, walifanya
mpango wa kuwaokoa watoto hao na kumkamata baba yao.
Alidai katika maisha
yao ya ndoa, mama wa watoto hao alizuiwa kuhudhuria kliniki wakati akiwa
mjamzito hivyo watoto wake wote watano alilazimika kujifungulia kwa wakunga wa
jadi .
“Watoto wote hawakuwahi kutibiwa
hospitali kwani baba yao alitaka watibiwe kwa dawa za kienyeji,” alidai Sunday.
Kwa mujibu wa Ofisa Ustawi wa Jamii Mbwete, watoto hao (majina tunayahifadhi) wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni kwa uchunguzi wa kitabibu.
“Nitakachokifanya ni kuhakikisha kuwa baada ya tiba watoto hawa wanakuwa katika mikono salama. Natoa rai kwa ndugu yeyote ambaye ana uwezo, kukaa nao, lakini wawe salama…baada ya hapo tutakuwa tukiwatembelea kuhakikisha kuwa kweli wanaendelea kuwa salama.” alisisitiza Mbwete.
Kwa mujibu wa Ofisa Ustawi wa Jamii Mbwete, watoto hao (majina tunayahifadhi) wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma, Maweni kwa uchunguzi wa kitabibu.
“Nitakachokifanya ni kuhakikisha kuwa baada ya tiba watoto hawa wanakuwa katika mikono salama. Natoa rai kwa ndugu yeyote ambaye ana uwezo, kukaa nao, lakini wawe salama…baada ya hapo tutakuwa tukiwatembelea kuhakikisha kuwa kweli wanaendelea kuwa salama.” alisisitiza Mbwete.
Mganga Mfawidhi wa
Hospitali hiyo, Dk Makris Yakayashi alisema baada ya uchunguzi wa kitabibu,
imebainika watoto hao wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu, utapia mlo mkali
na matatizo mengine ya kisaikolojia na upungufu wa kinga unatokana na kutopata
lishe ya uhakika.
Mama mzazi wa watoto
hao, Gauzia Zuberi alisema katika maisha yao ya ndoa, mumewe alikuwa akiwatesa
kwa kuwapiga, kuwanyima chakula na wakati mwingine kuwamwagia maji akidai
anawaogesha kisha kuwatembeza mtaani usiku kucha.
Credit: Habari leo
Credit: Habari leo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BABA AWAFUNGIA WATOTO NDANI MIEZI 10, WASHINDIA MLO MMOJA, MTOTO MMOJA AFA.”
Post a Comment