Tuesday, September 16, 2014
KAMPUNI YA SEED CO KUZAWADIA WANAFUNZI MADAWATI 100 YENYE THAMANI YA MIL 15 KATIKA SHINDANO LA SHAMBA DARASA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.
Do you like this story?
![]() |
Kaimu Meneja wa Seed Co Bw Michael Rikanga akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mashindano ya Shamba darasa |
![]() |
Kaimu Meneja wa Seed Co Bw Michael Rikanga akionyesha bango kwa Waandishi wa Habari jinsi ya kushiriki shindano hilo la shamba darasa |
![]() |
Waandishi wa Habari wakiwa makini kumsikiliza kaimu Meneja wa kampuni Seed Co. |
Katika kuhakikisha serikali inatimiza azma yake ya
kuwakomboa wakulima nchini hususani katika suala la kilimo bora cha
kibiashara taasisi binafsi zinazojiuhusisha na shughuli ya usambazaji
wa mbegu bora za kilimo zimeendelea na harakati za kuisaidia serikali
katika suala hilo.
Hatua hiyo ni pamoja na kutoa elimu pamoja na kusambaza
pembejeo bora za kilimo zenye kukidhi mahitaji ya mkulima.
Kutokana na hali hiyo kampuni ya Seed Co imezindua shindano
rasmi la mashamba darasa kwa shule za Msingi Tanzania ambazo zitaanza
mchakato wa kulima shamba darasa kwa kufuata kanuni bora za kilimo cha
kisasa .
Akizungumza jijini Mbeya Kaimu meneja wa Kampuni hiyo Kanda
ya Nyanda za juu Kusini Ndugu Michael Rikanga amesema shindano hilo ni
mahususi kwa shule za msingi za Mbeya Iringa Njombe na Ruvuma pamoja na
Rukwa na Katavi ambapo shindano hilo linatalajiwa kuanza msimu mpya wa kilimo
.
Amesema kwa shule itakayokuwa imelima shamba darasa zuri kwa
kuzingatia misingi yote ya kilimo bora cha kisasa itajishindia zawadi kubwa ya
madawati yenye thamani ya shilingi mili15.
Amesema pamoja na zawadi hiyo ya madati kwa
mshindi wa kwanza pia mshindi atapatiwa sare za michezo madaftari
na kalamu za kuandikia pamoja na mwalimu wa somo la kilimo kupatiwa simu ya
mkononi.
Amesema ili kushiriki mwanafunzi au mwalimu wanatakiwa
kutembelea maduka ya mawaka maalum waliothibitishwa na Kampuni hiyo ya Seed Co
ili kujisajili katika shindano hilo.
Hata hivyo Meneja huyo amesema kuwa katika hatua za uandaaji
na usimamizi wa shamba darasa Kampuni hiyo itatoa pemebejeo zote
zitakazohitajika ikiwa ni pamoja na mbegu za mahindi mbolea ya kupandia
na kukuzia .
Mahitaji mengine ni pamoja na madawa ya kupulizia
iwapo iwapo mazao yataonyesha dalili za kushambuliwa na wadudu waharibifu.
Lengo la kampeni hiyo kufundisha kilimo kwa njia ya
vitendo kwa wanafunzi wa shule za msingi sanjali na kutoa
nafasi kwa wanafunzi kujishindia zawadi kutoka katika kampuni hiyo ya Seed Co
Tanzania Limited.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KAMPUNI YA SEED CO KUZAWADIA WANAFUNZI MADAWATI 100 YENYE THAMANI YA MIL 15 KATIKA SHINDANO LA SHAMBA DARASA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.”
Post a Comment