Saturday, November 15, 2014
TRA MKOA WA MBEYA YATARAJIA KUADHIMISHA SIKU YA MLIPA KODI.
Do you like this story?
Meneja wa TRA Mbeya Anord Maimu
akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuanza kwa maadhimisho ya siku ya
Mlipa kodi inayotalajiwa kaunza Nov 17 hadi 21 mwaka huu.
|
MAMLAKA ya Mapato TRA Mkoa Mbeya
imewataka wafanyabiashara kutambua kuwa suala la matumizi ya mashine za
EFD lipo kisheria hivyo ni vema wakaitekeleza kuliko kuendelea kutupiana
lawama.
Imesema, bunge ndio lililopitisha
sheria hiyo na mamlaka inawajibika katika usimamizi na utoaji wa elimu
hivyo hakuna haja ya kuendelea na mvutano.
Kauli hiyo imetolewa na
Meneja wa mamlaka ya Mapato Mkoa wa Mbeya, Anord Maimu, wakati akizungumza na
waandishi juu ya kuadhimisha wiki ya mlipa kodi ambayo kila mwaa huadhimishwa
na mamla hiyo.
Amesema, mamlaka haitungi sheria
kwani sheria zote wanazozisimamia zimepitishwa na Bunge hivyo suala la mashine
lililipitishwa na bungeni na wenye wajibu wa kulitekeleza ni TRA.
Amesema, kazi kubwainayofanywa na
TRA ni kutoa elimu kwa wafanyabiashara juu ya matumizi ya mashine hizo pamoja
na umuhimu wake katika kuinua pato la Taifa kupitia mashine hizo.
Amesema wao kama mamlaka hawana
mvutao wowote na wafanyabiashara hao kama ambavyo imekuwa ikitafsiliwa na wengi
badala yake wao wamekuwa mstari wa mbele katika kuendelea kutoa elimu juu ya
matumizi ya mashine hizo.
Aidha, Maimu aliwataka
wafanyabiashara hao kuitumia vizuri siku ya mlipa kodi inayotarajia kuanza
November 17 mwaka huu na kilele chake kufanyika November 21 katika ukumbi wa
Mkapa.
Hata hivyo, alisema katika siku
hiyo TRA inakusudia kufanya shughuli mbalimbali zilizoambatana na utoaji huduma
kwa makundi muhimu ya jamii kama vile utoaji wa vyandarua 50 na shuka 50 katika
hospitali ya Wilaya ya Kyela.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TRA MKOA WA MBEYA YATARAJIA KUADHIMISHA SIKU YA MLIPA KODI.”
Post a Comment