Saturday, November 15, 2014
BASATA LAWATAKA WAANDAAJI WA MASHINDANO/MATUKIO YA SANAA KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZAO
Do you like this story?
Katika mazungumzo
maalum na Kituo cha Mlimani TV cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kaimu Katibu
Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Godfrey Mngereza amewasisitiza
waandaaji wa matamasha na mashindano ya Sanaa na urembo kuzingatia kanuni na
taratibu zilizopo katika kuendesha matukio yao.
Pia,amewataka
waandaaji wa mashindano na matamasha katika vitongoji kuwa makini katika
kusimamia taratibu kwani ndiyo wanaoandaa washiriki ambao baadaye wanakuja
kushiriki kwenye ngazi ya taifa.
Katika hili
amewataka kutumia upembuzi yakinifu kabla ya kuruhusu washiriki ama wasanii
kushiriki katika matukio yao ili kukwepa aibu kwa taifa.
"Kama
kuna vielelezo au nyaraka zinahitajika, waandaaji lazima waziombe kwa washiriki
na wazihakiki kikamlifu. Kama kuna utata wahakikishe wanahusisha mamlaka
zinazohusika mapema ili kuupata ukweli" aliongeza Mngereza.
Aidha, amesisitiza
kwamba BASATA litaendelea kuwabana waendeshaji/waandaaji wa matukio ya Sanaa
kwani ndiyo wenye jukumu la kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa na ndiyo
wanaopewa idhini ya uendeshaji na Serikali.
“Kama katika
ngazi ya vitongoji,wilaya na kanda waandaaji wangeweka msisitizo, changamoto
zisingekuwepo. Kuna ulegelege wa kudhibitiwa” Aliongeza.
Amewataka
waandaaji wote kusimamia kanuni na taratibu zao kwa haraka pasipo
kusubili mashinikizo na malalamiko kutoka kwa jamii.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BASATA LAWATAKA WAANDAAJI WA MASHINDANO/MATUKIO YA SANAA KUZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZAO”
Post a Comment