Friday, September 15, 2017

WATU WANNE WAFARIKI KATIKA AJALI MBEYA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA
Mwonekano wa Gari aina ya Coaster iliyopata ajali.




                                                       

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI “PRESS RELEASE” TAREHE 15.09.2017.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaongeza jitihada za kuzuia na kupunguza matukio ya ajali za barabarani kwa kuhakikisha madereva na watumiaji wengine wa barabara wanafuata sheria na alama za usalama Barabarani. Aidha kumekuwa na ajali 01 ya vifo kama ifuatavyo:-

Mnamo tarehe 14.09.2017 majira ya saa 19:45 usiku huko eneo la Mlima Iwambi, Kata ya Songwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya kwenda Tunduma, kulitokea ajali iliyohusisha magari matano yenye namba za usajili T. 231 BME aina ya Tipper ikiendeshwa na dereva FRED MWAKALINGA [33] Mkazi wa Itiji - Mbeya ikitokea Mbeya mjini kwenda Mbalizi, Gari yenye namba za usajili T. 515 ARE aina ya Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na dereva EMMANUEL JULIUS [29] Mkazi wa Itiji ikitokea Mbalizi kwenda Mbeya mjini, Gari yenye namba za usajili T.126 DJZ aina ya Fuso basi iliyokuwa ikiendeshwa na AMOS MWAIKAJA @ CHODO [40] Mkazi wa Kagera – Soweto, Gari yenye namba za usajili BCA 8730 na tela BCA 8733 ikiendeshwa na EVANS MUSONDA [39] raia wa Zambia na Gari yenye namba za usajili T.570 CKC aina ya Toyota dyana ikiendeshwa na dereva AMOS BENSON pamoja na Pikipiki moja ambayo haijafahamika namba zake za usajili ikiendeshwa na dereva aitwaye JANIA JACKOBO @ SANGA [27] Mkazi wa Iwambi.

Katika ajali hiyo watu wanne walifariki dunia ambao ni dereva wa Gari yenye namba za usajili T.570 CKC AMOS BENSON, mwendesha Pikipiki ambayo bado hajafahamika namba zake za usajili aitwaye JANIA JACKOBO @ SANGA [27] Mkazi wa Iwambi, dereva wa Gari lenye namba za usajili BCA 8730/BCA 8733 EVANS MUSONDA [39] raia wa Zambia na Mwanamke mmoja ambaye bado hajafahamika ambaye alikuwa abiria kwenye Gari yenye namba za usajili T.570 CKC Toyota Dyana.

Aidha katika ajali hiyo, watu wengine tisa walijeruhiwa kati yao wanaume ni wanne na wanawake watano. Aidha kati ya majeruhi hao, wawili wamelazwa Hospitali ya Rufaa Mbeya na saba wamelazwa Hospitali Teule Ifisi - Mbalizi. Chanzo cha ajali kinachunguzwa hata hivyo inahisiwa kuwa dereva wa lori alikosa umakini na kuanza kugonga magari mengine ambaye pia amepoteza maisha katika ajali hiyo. Upelelezi unaendelea ili kubaini chanzo halisi cha ajali na dereva aliyehusika.

WITO:

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA anatoa wito kwa Madereva kuwa makini wanapotumia vyombo ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika. Aidha Kamanda MPINGA anawataka madereva kufuata, kuheshimu na kuzingatia sheria na alama za barabarani ili kuepuka ajali.

                                              Imesainiwa na:
 [MOHAMMED R. MPINGA - DCP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

0 Responses to “WATU WANNE WAFARIKI KATIKA AJALI MBEYA ”

Post a Comment

More to Read