Sunday, February 8, 2015
KISA BOKO HARAM, UCHAGUZI MKUU NCHINI NIGERIA WAAHIRISHWA.
Do you like this story?
Wananchi wakiwa na mabango ya kupinga kuahirishwa kwa uchaguzi huo. |
TUME
ya uchaguzi nchini Nigeria imeahirisha uchaguzi mkuu ambao ulikuwa ufanyike
tarehe 14 mwezi huu kutokana na sababu za kiusalama.
Uchaguzi
huo sasa utafanyika Machi 28 mwaka huu.
Mkuu
wa tume hiyo Attahiru Jega alisema kuwa amejulishwa na maofisa wa usalama kuwa
wanajeshi hawatakuwepo kulinda vituo vya kupigia kura kwa kuwa watakuwa
wakipigana na wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi.
Awali
tume hiyo ilikuwa imetangaza kuwa haingewezekana kufunguliwa kwa vituo vya
kupigia kura katika maeneo ambapo maelfu ya watu tayari walikuwa wamehama.
Mwandishi
wa BBC anasema kuwa kuahrishwa kwa uchaguzi kutaleta utata kwa kuwa chama kikuu
cha upinzani kimekashifu jeshi kwa kulazimisha kuahirishwa kwa uchaguzi huo ili
kumsaidia rais Goodluck Jonathan kufanya kampeni.
Credit:
BBC
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KISA BOKO HARAM, UCHAGUZI MKUU NCHINI NIGERIA WAAHIRISHWA.”
Post a Comment