Monday, February 9, 2015
MKULIMA, MWALIMU WASHINDA MAGARI YA AIRTEL YATOSHA ZAIDI.
Do you like this story?
Washindi hao kila mmoja ameibuka mshindi wa gari aina ya IST
Toyota mpya, ikiwa ni siku chache tu tangu kuzindulia kwa promosheni hiyo.
Airtel Tanzania wiki iliyopita ilitangaza dhamira yake ya
kuwazawadia wateja wake wanaojiunga na bando za Airtel Yatosha gari
moja kila siku kwa siku 60 ambapo mwishoni mwa wiki tayari magari matatu
yalipata washindi.
Balozi wa Airtel, na msanii maarufu wa filamu nchini,
Elizabeth Michael ‘Lulu’, ndiye aliyekuwa na jukumu la kuwapigia simu washindi
na kuwapa taarifa hizo nzuri kwa mwaka 2015 chini ya Mkaguzi Mwandamizi kutoka
Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid
Wa kwanza kupigiwa alikuwa Namtapika Kilumba wa Mtwara mwenye
umri wa miaka 60 na aliposikia sauti ya Lulu ikisema; “Ninapenda kukutaarifu
kuwa umeshinda gari aina ya IST Toyota mpya baada ya kujiunga na Airtel Yatosha
Zaidi”, alipiga kelele kwa furaha na mara moja akamshukuru Mungu pamoja na
Lulu.
“Mungu wangu. Sikutarajia kabisa kama leo ningepata taarifa
nzuri kama hizo! Kumbe ni kweli kuwa mtu yeyote anaweza kushinda promosheni ya
Airtel? siamini,” alisema … kwa njia ya simu; na hata wengine pia waliopigiwa
simu na Lulu walikuwa na maoni yanayoshabihiana na hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya droo hiyo,
Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando, alisema: “Haya ndio kwanza magari
matatu tu. Bado mengine 57 yote aina ya IST Toyota mapya kabisa yapo
‘showroom’. Ndani ya 60 za mwaka huu, wateja 60 wa Airtel watakuwa wakiishi
maisha mapya katika dunia ya ndoto zao.
“Watakuwa ni wamiliki wa magari kwa kujiunga na bado za
Airtel Yatosha zaidi kwa kupiga simu *149*99# na kujiunga. Hebu fikiria,
unapata muda wa maongezi zaidi, vifurushi vya internet zaidi, SMS zaidi na bado
unakuwa na nafasi ya kujishindia gari.”
Mmbando alimtaja mshindi mwingine kuwa ni Mwajabu Churian
mwenye umri wa miaka 27 na mfanyabiashara anaeishi Mbagala huku akiwasihi
wateja wa Airtel kuendelea kufurahia huduma hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MKULIMA, MWALIMU WASHINDA MAGARI YA AIRTEL YATOSHA ZAIDI.”
Post a Comment