Wednesday, February 25, 2015

MKUU WA MKOA WA NJOMBE ASHAURI MAVAZI YA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI KUBADILISHWA


Aliyekuwa  mkuu wa  mkoa wa Njombe Kepten  Mstaafu Aser
Msangi akikagua  wanafunzi  wa  shule  ya  msingi Ninga  ambao
wanatumia  sare za mkaptula




Dr Nchimbi alitoa rai   hiyo  leo  wakati  wa  ufunguzi  wa  kikao  hicho  cha RCC na  kuongeza  kuwa  kutokana na hali ya   hewa  ya  baridi   kali   mkoa  wa Njombe ni  vema  viongozi  mkoani  hapa  kuangalia uwezekana  na  kufanya mabadiliko ya sare  hizo  za  wanafunzi  ili  kuvaa suruali.

Alisema   kuwa hali ya  hewa  ya  mkoa  wa  Njombe  ni hali ya  baridi  kali  hivyo kuna haja  ya  wanafunzi  hao  kulinda kiafya  zaidi kwa  kubadilishiwa  sare  hizo  ili  kuvaa  suruali  kwa  ajili ya  kujisitili na baridi  kali .

"Ndugu  wajumbe  mkoa   wetu  ni mkoa  wenye  baridi  kali  hivyo  kuendelea  kuwaacha  watoto  wetu  kutumia  sare  hizi  za kaptula  ni  kuwatesa  zaidi ......naona  si  vibaya   kubadili   sare  na  wizara  ya  elimu na mafunzo  ya  ufundi  kuelezwa  sababu   hii mbona   wanaume  wa Njombe  kutokana na baridi  hii  wanavaa suruali tena  wengine  wanavaa mbili  zaidi sasa  iweje  watoto  wetu  kuendelea  kuteseka na baridi"alisema

Katika  hatua  nyingine  mkuu  huyo  wa  mkoa alitaka viongozi  wa  mkoa  wa  Njombe kuwa na  jibu  moja kwa swali la ujenzi  wa maabara na uhaba  wa madawati  kwa  kila  wanapoulizwa  waseme  wamekamilisha ujenzi  huo  wa maabara mbali ya  kuwa  wamekarabati  vyumba vya madarasa yaliyokuwepo.

" Naomba tuwekane  sawa hapa  kuna  vijimaneno maneno vimeanza  kusikika  kuwa hatujakamilisha ujenzi  wa maabara ukweli  sisi  tumetumia  mbinu  zetu  kukamilisha  maabara  kama  tumegeuza  vyumba  vya  madarasa hiyo  ni  mbinu  yetu  wao  walitaka maabara na maabara  zote  zipo  na  sisi  hatuna upungufu  wa vyumba  vya madarasa  wala maabara "

Wakati  huo  huo  serikali ya  mkoa  wa  Njombe  imewataka  viongozi  wanaohusika na  migao  ya  fedha  za  uondeshaji  wa  mikoa kuutazama mkoa  wa  Njombe kwa  jicho la tatu  ili  mgao  wake  uwe  mkubwa  zaidi kama  njia ya  kuuwezesha mkoa  huo  kusonga  mbele  mbele kimaendeleo.

Mkuu  wa  mkoa  wa  Njombe Dr Nchimbi  alisema  kimsingi mtoto ndie  anayepata  mahitaji  bora  ili apate  kukua  hivyo mkoa  wa  Njombe  wenye utajiri  mkubwa wa chuma na makaa ya mawe  unahitaji  kutengewa bajeti  kubwa  zaidi  ili  kuweza  kupita hatua  na  kuweza kuwa  mkoa  wa kiuchumi  kwa Taifa.

0 Responses to “MKUU WA MKOA WA NJOMBE ASHAURI MAVAZI YA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI KUBADILISHWA ”

Post a Comment

More to Read