Friday, February 13, 2015
MKUU WA WILAYA YA MUFINDI IRINGA NA WAKURUGENZI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA RUSHWA
Do you like this story?
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na
Rushwa (Takukuru), jana iliwapandisha mahakamani Mkuu wa Wilaya ya Mufindi,
Evarista Kalalu na wakurugenzi wawili kwa makosa mawili yanayohusiana na rushwa
kinyume na Kifungu cha 32 cha Sheria ya Takukuru Namba 11 ya mwaka 2007.
Katika kesi hiyo inayowaunganisha
maofisa wengine wawili wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi, wanatuhumiwa
kuisababishia halmashauri hasara ya Sh milioni 3.
Kesi hiyo iliyopewa jina la kesi ya
uhujumu uchumi namba moja ya mwaka 2015, ilifunguliwa jana katika Mahakama ya
Wilaya ya Mufindi mkoani hapa.
Mkuu wa wilaya hiyo na watuhumiwa hao
wengine kwa pamoja wamekana mashitaka yao mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama
hiyo, Victoria Nongwa.
Watuhumiwa wengine katika shitaka hilo
ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mikindani mkoani Mtwara, Limbakisye
Shimwela ambaye wakati kosa hilo likitendeka kati ya Desemba 2010 na Februari
2011, alikuwa Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi na mwingine ni
Mkurugenzi wa halmashauri ya Biharamulo mkoani Kagera, Nasibu Bakari.
Watuhumiwa wengine waliofikishwa katika
mahakama hiyo, kutokana na ushiriki wao wa makosa katika kesi hiyo ni Ofisa
Mipango wa Halmashauri ya Mufindi, Cosmas Mduda na Fundi Ujenzi wa wilaya hiyo,
Fedrick Zaveri.
Akisoma shitaka linalowakabili
watuhumiwa hao mahakamani hapo, Mwendesha mashitaka wa Takukuru Mkoa wa Iringa,
Imani Mizizi alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo kuwa kati ya
Desemba 2010 na Februari 2011 watuhumiwa hao kwa pamoja walikula njama ya
kutenda kosa la rushwa kinyume na kifungu cha 32 Sheria ya Kuzuia na Kupambana
na rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.
Katika kosa la pili, linalowakabili
watuhumiwa watatu katika kesi hiyo, ambao ni Shimwela ambaye ni Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Mtwara/Mikindani, Bakari ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Biharamulo na Cosmas ambaye ni fundi ujenzi, ni lile la matumizi
mabaya ya ofisi kinyume na kifungu cha 31 cha sheria kuzuia na Kupambana na
Rushwa.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa kati ya
Desemba 2010 na Februari 2011, watuhumiwa hao watatu walitumia ofisi vibaya kwa
kuingia mkataba na Fedrick Zaveri kwa ajili ya ujenzi wa vyoo, bafu za kuogea
na mfumo wa maji katika shule ya sekondari ya Ihalimba bila kufuata Sheria ya
Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004.
Ilidaiwa kuwa kutokana na ha Watuhumiwa
wote wamekana kosa na kuachiwa kwa dhamana baada ya kukidhi masharti ya kila
mmoja kuwa na wadhamini wawili na bondi ya Sh milioni moja kwa kila mdhamini.
Hakimu Victoria aliahirisha kesi hiyo
hadi Machi 13 mwaka huu, watu hao watakapokuja kusomewa maelezo ya awali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MKUU WA WILAYA YA MUFINDI IRINGA NA WAKURUGENZI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA RUSHWA ”
Post a Comment