Wednesday, February 18, 2015
RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA WAPYA 27, PAUL MAKONDA NA FREDRICK MWAKALEBELA NDANI
Do you like this story?
Mkuu mpya wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda. |
Mkuu mpya wa Wilaya ya Wanging’ombe, Fredrick Wilfred Mwakalebela. |
RAIS
Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Wakuu wapya
27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao
vya kazi vya zamani.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa OWM TAMISEMI leo mchana (Jumatano,
Februari 18, 2015) Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo
yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa
wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano,
kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa
wakuu wa wilaya 12.
Hata
hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa
wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.
Wakuu
wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa;
Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili
Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Fredrick
Wilfred Mwakalebela anayeenda wilayaya Wanging’ombe.
Wengine
na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga
(Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi
(Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S.
Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela);
Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Shaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).
Wengine
ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga
(Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa
Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah
Ally Mohamed (Serengeti).
Wakuu
wa Wilaya saba ambao uteuzi wao umetenguliwa lakini watapangiwa kazi nyingine
ni Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga
(aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa
Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa
Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).
Waziri
Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na
sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye
mabano kuwa ni James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro);
Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo
Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba
(Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J.
Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).
IMETOLEWA
NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015.
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA WAPYA 27, PAUL MAKONDA NA FREDRICK MWAKALEBELA NDANI”
Post a Comment