Wednesday, February 18, 2015
MVUA YAHARIBU HEKTA 62 ZA MAHARAGE MBOZI.
Do you like this story?
Na Saimeni
Mgalula,Mbeya
Jumla ya hekta
62 za Maharage pamoja na 148 mahindi na 168 za kahawa zimeharibiwa vibaya
kutokana na mvua kubwa iliyonyesha katika kijiji cha Isansa Wilaya Mbozi Mkoani
Mbeya.
Mvua hiyo
ilinyesha takribani dakika 45 ambayo ilianza kunyesha kuanzia saa 9:00 mpaka
9:45 arasili ambapo ’iliambatana na mawe makubwa na kusababisha uhalibifu
huo .
Kutokana na
hali hiyo Wakazi wa kijiji hicho wameiomba serikali kuwapatia msaada wa
chakaula cha mahindi kutokana na Mazao yao kuharibiwa na mvua hiyo .
Akizungumzia
maafa hayo ,Afisa kilimo wa Wilaya ya Mbozi Richard Silinde amesema inawezekana
kukawa na njaa kutokana na mvua hiyo kuharibu mazao kwa kiasi kikubwa sana katika
kijiji hicho.
Amesema
mazao ambayo yameharibiwa na mvua hiyo ni Kahawa ,Mahindi ambayo yalikuwa
yanaanza kubeba watoto na Zao la Maharage ambalo ndio limeharibiwa vibaya.
Amesema kuwa pia
kuna baadhi ya Kaya ziliaribiwa na mvua hiyo kwa kutobolewa mabati ambayo
yameezekwa ambapo pia hakukuwa na madhara yeyote kwa binadam.
Afisa huyo
amesema kutokana na maafa hayo Serikali inafanya taratibu kwa kina juu ya
tatizo hilo na mara baada ya kumaliza taratibu hizo tutawakilisha taarifa nzima
katika kamati ya Pembe Jeo ili baadhi ya wakulima wapewe mbegu kutokana
na kuwepo kwa mbegu fupi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MVUA YAHARIBU HEKTA 62 ZA MAHARAGE MBOZI.”
Post a Comment