Saturday, February 21, 2015
WATOTO WENGINE WATEKWA SUDANI KUSINI.
Do you like this story?
Umoja wa mataifa unasema kuwa vijana kadha, wengine wa
umri wa miaka 13 tu, wametekwa nyara Sudan Kusini.
UNICEF
inaeleza kuwa kama 89 walitekwa na wanaume waliokuwa na silaha ambao walipita
majumbani kutafuta watoto wa kiume wa zaidi ya miaka 12.
Baadhi
yao walinyakuliwa wakati wanafanya mitihani.
Mambo
hayo yalitokea kwenye kambi katika jimbo la kaskazini la Malakal, ambalo lina
maelfu ya watu waliokimbia vita baina ya wanajeshi wa serikali na wapiganaji.
Pande
zote mbili katika vita hivyo wametuhumiwa kuwa wanatumia watoto vitani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATOTO WENGINE WATEKWA SUDANI KUSINI. ”
Post a Comment