Saturday, February 21, 2015
NAUNGANA NA WEWE KUPINGA VITENDO VYA KIKATILI JUU YA ALBINO.
Do you like this story?
"Ni kweli mimi ni
Albino, nimejikubali na nimeishi maisha yangu yote bila kujali nilivyo.
Sijawahi kutumia hali yangu kupata kitu kwa huruma, nimeyapigania maisha yangu
na nimepiga hatua.
Leo hii naongea nanyi
nikiwa Baba, Mume, Mwandishi Mwandamizi, Blogger, na mengine mengi, lakini hali
yangu sasa inaanza kunikwaza.
Haya mauaji jamani,
nimejiteua kuwa Balozi, nitatetea, na kusimama mbele ya wenzangu wote wenye
hali kama hii, kama ni wanasiasa ama wafanyabiashara, wanataka kutuua kwa
maslahi binafsi, mwaka huu HAPANA.
Wanaoniunga mkono
mikono juu" Mwisho wa kunukuu.
Nikiwa kama Blogger na
Mwanahabari Mwenza wa rafiki yangu na Kaka yangu Kipenzi,Henry Mdimu
aliejitolea kuwa Balozi,nanyoosha mkono juu kwa kuunga mkono kupiga vita vikali
mauaji ya ndugu zetu wenye Albinism.kwani wao pia ni Binadamu kama tulivyo mimi
na wewe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “NAUNGANA NA WEWE KUPINGA VITENDO VYA KIKATILI JUU YA ALBINO.”
Post a Comment