Wednesday, September 30, 2015
NYOSSO APEWA KIFUNGO NA FAINI JUU BAADA YA KUMDHALILISHA BOCCO
Do you like this story?
Kikao cha Kamati ya
nidhamu ya TFF kilichokutana ndani ya saa 72, kimefungia nahodha wa Mbeya City,
Juma Said Nyosso kucheza soka kwa miaka miwili.
Pamoja na miaka hiyo
miwili, Nyosso ametozwa faini ya Sh milioni mbili kutokana na kitendo chake cha
kumshika makalio nahodha wa Azam FC, John Bocco.
Hii ni mara ya pili
kwa Nyosso kushiriki katika tukio, mara ya kwanza alimtomasa Elius Maguli
wakati akiichezea Simba.
Kutokana na picha
ilivyochapishwa kwenye gazeti la Championi na SALEHJEMBE akafungiwa kucheza
mechi nane.
Baada ya hapo, Nyosso
aliwaomba radhi Watanzania pamoja na wapenda soka wote, lakini bado amerudia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ NYOSSO APEWA KIFUNGO NA FAINI JUU BAADA YA KUMDHALILISHA BOCCO”
Post a Comment