Wednesday, September 23, 2015
VITUO VYA RADIO NA TV ZOTE NCHINI VYAONYWA NA TCRA
Do you like this story?
Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vituo vya redio na televisheni nchini
Tanzania kuepuka kurusha habari za uchochezi hasa katika kipindi hiki cha
kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk. Ally Simba ameeleza
kuwa vyombo vya habari vinatakiwa kuepuka kurusha na kuandika habari
zitakazochochea vurugu na uvunjifu wa amani kwan jamii ina imani kubwa na
vyombo vya habari na waandishi wa habari, hivyo hawana budi kutumia weledi katika
utoaji wa taarifa katika kipindi hiki cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.
Radio 106 na televisheni 28, zimesajiliwa nchini
Tanzaia na kwamba katika kuelekea uchaguzi mkuu, tayari vituo vitano vya
televisheni vimekuwa na makosa yaliyosababisha kupewa adhabu na onyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “ VITUO VYA RADIO NA TV ZOTE NCHINI VYAONYWA NA TCRA”
Post a Comment