Thursday, October 22, 2015
.BAADHI YA WANANCHI WAHOFIA UCHAGUZI NA KUHAMA MAKAZI YAO KWA MADAI KUWA MITA 200 MTWARA
Do you like this story?
Wananchi
wa mkoa wa Mtwara wameingia hofu na baadhi yao wameanza kuyakimbia makazi yao
wengi wakiwa wanawake na watoto kwa madai nyumba zao zipo ndani ya mita
miambili hivyo wanalazimika kuondoka kutii kauli ya serikali.
Wakizungumza na
waandishi baadhi ya wananchi wamesema mbali na kutii kauli hiyo wingi wa askari
polisi ambao wamesambaa maeneo mbalimbali ya mji wamekuwa wakitia hofu
wananchi.
Akizungumzia
hofu hiyo mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego amesema jeshi la polisi
limelazimika kuweka ulinzi huo baada ya kuwapo kwa taarifa za kuandaliwa
makundi mbalimbali kuzuia watu kupiga.
Watu laki saba
ishirini na nane elfu na mia tisa 81 kutoka majimbo kumi ya mkoa wa Mtwara
wanatarajiwa kupiga kura siku ya jumapili kuchagua rais, wabunge na madiwani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “.BAADHI YA WANANCHI WAHOFIA UCHAGUZI NA KUHAMA MAKAZI YAO KWA MADAI KUWA MITA 200 MTWARA”
Post a Comment