Monday, October 12, 2015
.NEC YAOMBWA KUWEKA WAZI HATUA ZOTE ZA UPIGAJI KURA HADI MATOKEO
Do you like this story?
Mkuu wa Mkoa wa Kagera,John Mongella |
Katika
kuondokana na malalamiko ambayo hujitokeza baada ya uchaguzi ambayo
hupelekea baadhi ya wagombea na viongozi wa vyama vya siasa kutokubaliana
na matokeo hali ambayo wakati mwingine husababisha vitendo vya uvunjifu wa
amani, tume ya taifa ya uchaguzi imeombwa kuweka wazi hatua zote zitakazoongoza
mchakato wa zoezi wa upigaji kura hadi hatua ya kutangaza matokeo.
Ombi hilo
limetolewa na mkuu wa mkoa wa kagera,John Mongella kwenye hotuba yake aliyoitoa
wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa maofisa wasimamizi wa uchaguzi
wa mikoa ya Geita na Kagera iliyoandaliwa na tume ya taifa uchaguzi na
kufanyika kwenye hoteli ya Kolping iliyoko katika manispaa ya Bukoba.
Kwa upande
wake,Raphael Nswanzigwanko ambaye ni mratibu wa uchaguzi wa mikoa wa kanda ya
ziwa ameeleza kuwa tume ya taifa ya imejipaga vizuri na itahakikisha
uchaguzi mkuu unakuwa huru na wa haki, pia amewatahadhalisha wananchi kuwa
makini na watakaotoka matokeo kwa kutuma njia zao amesema tume hiyo ndiyo
yenye mamlaka ya kutangaza matokeo.
Naye, msimamizi
wa wa uchaguzi wa mkoa wa Kagera,Fabian Kapucholojiga anaeleza maandalizi ya
uchaguzi ambayo yameishafanyika hadi sasa katika mkoa huo, huku Aron
Kagulumjuli mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya bukoba, akieleza changamoto
ambazo wasimamizi wa uchaguzi hukumbana nazo mara kwa mara ambazo zinatakiwa
kupatiwa ufumbuzi wa haraka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “.NEC YAOMBWA KUWEKA WAZI HATUA ZOTE ZA UPIGAJI KURA HADI MATOKEO”
Post a Comment